
Picha
ya chini na juu ni baadhi ya majeruhi walikuwa kwenye basi hilo aina
ya Urio lililopata ajali leo jioni katika eneo la Kia wilayani Hai
mkoani Kilimanjaro
wananchi
wawakiwa wanashuhudia ajali hiyo iliotokea leo jioni katika eneo la kia
ambapo inasemekana watu zaidi ya 31 wamejeruliwa
Basi
aina ya Urio yenye namba za usajili T 137 BCX inayofanya safari zake
moshi kuelekea leguruki mkoani Arusha leo limepinduka katika eneo la
kia na kujeruhi watu zaidi ya 31
kwa
mujibu wa mashuhuda waliokuwepo katika eneo la tukio walisema kuwa
dereva huyo alikuwa anajaribu kukwepa pikipiki iliyokuwa imejichomeka
barabarani
"dereva
huyu alikuwa anajaribu kukwepa pikipiki ndipo gari ikamshinda na kuama
barabara ndipo ilipo anguka gafla na kubiringita mara tatu apa yenyewe
unavyoiyona tumeigeza ilikuwa kichwa chini matairi juu"alisema mmoja
wapo wa shuhuda ambaye akutaka kutaja jina
mpaka
kamera ya libeneke la kaskazini inaondoka eneo la tukio watu 31
walikuwa wamekwishwa pelekwa katika hospitali ya wilaya ya hai kwa ajili
ya matibabu wakiwemo wanafunzi wa shule ya leguruki ambao walikuwa
wanarejea shuleni mara baada ya kumaliza likizo yao ya sikukuu ya
pasaka
CHANZO LIBENEKE LA KASKAZINI
Post a Comment