Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS MAGUFULI NA HISTORIA ISIYOFUTIKA



Na Emmanuel J. Shilatu

Kama ambavyo Watanzania tunavyomkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa kusaidia ukombozi wa upatikanaji wa uhuru ama kama ambavyo Hayati Moringe anavyokumbukwa kwa mapambano ya ubadhirifu wa mali za umma, pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anazidi kujenga historia ya kipindi chote isiyofutika kutokana na utendaji, uchapakazi na uzalendo wake kwa Taifa.

Haya hapa ni baadhi ya Mambo ya kihistoria na yenye heshima kubwa kwa Taifa ambayo Rais Dkt. Magufuli aliyoyafanya;-

*(i) Kuhamia Dodoma*

Wazo la Serikali kuhamia kwenye makao makuu ya nchi mkoani Dodoma liliasisiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere mwaka 1973 lakini lilishindwa kutekelezwa katika awamu zote. Si awamu ya kwanza, wala ya pili, ama ya Tatu au ya nne bali limeweza kufanikiwa kwenye utawala wa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli. Leo hii karibia Serikali yote imehamia Dodoma. Wizara, taasisi na idara za Serikali, Waziri Mkuu wameshahamia Dodoma. Mwishoni mwa mwaka huu Rais Magufuli naye atahamia Dodoma. Iliasisiwa na Mwalimu Nyerere, ikahaidiwa kwenye ilani ya uchaguzi, imekuja kutekelezwa vyema na Rais Magufuli. Hii ni historia isiyofutika ya uthubutu, uzalendo alionao Rais Magufuli.

*(ii) Ujenzi wa Miundombinu*

Hili halina ubishi kwa asilimia kubwa kabisa miundombinu ya nchi hii imejengwa chini ya usimamizi wa Dkt. Magufuli toka alipokuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Waziri wa Ujenzi na sasa Rais wa nchi. Hauwezi ukazungumzia uwepo wa mitandao ya barabara nchi nzima pasipo kumtaja Rais Magufuli; hauwezi kuzungumzia uwepo wa madaraja makubwa ya kisasa kama ya Daraja la Nyerere, Daraja la Mkapa pasipo kumtambua mchango wa Rais Magufuli. Leo hii nchini tunajivunia uwepo wa flyovers. Rais Magufuli ameonyesha uwezo na heshima kubwa ya ujenzi wa Miundombinu nchini ambayo imekuwa msaada mkubwa wa kimawasiliano, usafirishaji wa Watu na mizigo, kukuza utalii, kuimarisha shughuli za kibiashara na kuongeza mapato ya nchi.

*(iii) Kulifufua Shirika la Ndege*

Tangu mwaka 1977 nchi yetu ilikuwa na shirika la ndege linalosua sua na linalojiendesha kihasara kubwa. Mara baada ya Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli imefanikiwa kununua ndege mpya 7 na mpaka sasa zimeshawasili ndege mpya 4 ikiwamo ndege kubwa aina ya Boeing 787-8. Wale baadhi wanaosema ndege si kipaumbele wala muhimu kwa Watanzania inabidi watambue Leo hii makusanyo ya mapato ndani ya Shirika la ndege (ATCL) yametoka Tsh. Milioni 700 mpaka kufikia Tsh. Bilioni 4.5. Hii ndio faida ambayo Watanzania tumeipata ya kuwa na kiongozi mwenye maono na mtazamo wa mbali zaidi, Rais Magufuli.

*(iv) Ujenzi wa Stiegler’s Gorge*

Utawala wa awamu ya kwanza uliokuwa ukiongozwa na Mwalimu Nyerere ulikuja na wazo wa kujenga Stiegler’s Gorge mnamo mwaka 1981 lakini umeshindwa kufanyika mpaka awamu hii ya 5 inayoongozwa na Rais Magufuli umeamua kufufua na kuliendeleza wazo hili. Mradi wa Stiegler’s Gorge kupitia Mto Rufiji utafanikiwa kuzalisha Megawattz 2100 utakapo kamilika. Ukamilifu wa mradi huu utajenga uhakika wa umeme nchini, utashusha bei ya umeme nchini na pia utamjengea Rais Magufuli heshima kubwa isiyofutika.

*(v) Mapambano dhidi ya Rushwa na ufisadi nchini.*

Rais Magufuli ameingia kwenye historia ya kiongozi ambaye Serikali anayoiongoza kuwa na mapambano ya dhahiri ya rushwa na ufisadi nchini. Tumeshuhudia Mafisadi Papa ambao walikuwa hawashikiki wala kukamatika wakipandishwa Mahakamani. Katika miaka ya nyuma ilikuwa suala gumu sana kwa Watuhumiwa “Mapapa” kuguswa tu, achilia mbali kupandishwa Mahakamani. Haya ni mapambano ya wazi wazi ya Serikali ya Rais Magufuli ya vita dhidi ya rushwa na ufisadi nchini. Leo hii Tanzania imepanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 na pia ikishika nafasi ya pili (2) kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

*(vi) Uwazi wa taarifa na udhibiti wa rasilimali za nchi*

Tumeshuhudia Serikali ikiweka uwazi kwenye mikataba na uchunguzi wa rasilimali za Taifa na kuweka makubaliano mapya yenye tija Mathalani tumeona uwazi wa sekta ya madini ya dhahabu, almas na Tanzanite ambapo Taifa tumeona namna ambavyo tulivyokuwa tukiibiwa na Serikali kuweka mikakati mipya ya kutokuibiwa tena. Kama haitoshi tumeshuhudia wawekezaji wakibanwa vilivyo juu ya mikataba isiyokuwa na tija kwa Taifa. Ni Serikali ya Rais Magufuli iliweka uthubutu wa kuwabana wawekezaji wa madini wa ACACIA iliyozaa matunda kwa Serikali ya Tanzania kumiliki asilimia 16 ya hisa katika makampuni ya uchimbaji wa madini, Serikali kupata gawio la faida ya madini ya asilimia 50 kwa 50. Yote haya yamewezekana kwa sababu ya uzalendo wake Rais Dk. Magufuli

*(vii) Ujenzi wa Bomba la Mafuta*

Serikali ya Rais Magufuli imefanikisha vilivyo kushirikiana na nchi ya Uganda kujenga Bomba la Mafuta linalotoka nchini Uganda mpaka Tanga nchini Tanzania. Ujenzi huo wa bomba la mafuta utazalisha ajira nchini na utaongeza pato la Taifa. Hayo yote yamefanikiwa kutokana na Serikali ya Rais Magufuli kuzidi kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi nyinginezo.

*Itaendelea …..*

*Shilatu E.J*

0767488622

Ufafanuzi wa TCRA kuhusu kuondoa chaneli za runinga zinazotazamwa bila kulipia (FTA) kutoka ving'amuzi vya Azam, Multichoice na Zuku

Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) imefafanua kuhusu kuondoa Channel za Televisheni za ndani zinazotazamwa bila kulipia (FTA) kutoka Ving’amuzi vya Azam, Multichoice na Zuku.



TRA: Msamaha Wa Riba Na Adhabu Ya Malimbikizo Ya Kodi Kutoa Motisha Kwa Wafanyabiashara Nchini


Na Veronica Kazimoto
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa msamaha wa riba na adhabu wa asilimia 100 kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi unaotolewa ndani ya Mwaka wa Fedha 2018/19 utawasaidia wafanyabiashara kulipa kodi ya msingi na hatimaye kuwapa motisha ya kulipa kodi kwa hiari na kwa wakati.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Kamishna wa Walipakodi Wakubwa wa mamlaka hiyo Alfred Mregi wakati akifungua semina elekezi ya msamaha wa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya kodi kwa wafanyabiashara iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mregi amesema kuwa dhumuni la semina hiyo elekezi ni kutoa uelewa wa kutosha kwa wafanyabiasha ili waweze kuwasilisha maombi yao kwa usahihi kwa lengo la kupatiwa msamaha huo.

"Leo tumekutana mahali hapa kwa lengo la kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu msamaha wa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi ili kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wote wenye malimbikizo ya madeni wananufaika na msahamaha huo unatolewa kwa asilimia 100," alisema Mregi.

Naye Naibu Kamishina wa Kodi za Ndani Abdul Zuberi amesema suala la kodi halijachwa kwa TRA peke yake bali taasisi zote za Serikali zinafanya kazi hiyo ya kuhamasisha ulipaji kodi kwa maendeleo ya watanzania wote.

"Sasa hivi kodi za ndani zimezidi kuongezeka kutokana na uhamasishaji ambao unatoa motisha kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kulipa kodi kwa maendeleo ya taifa letu," alieleza Zuberi.

Kwa upande wake Mfanyabiashara mkubwa kutoka kampuni ya Super Group of Companies inayozalisha sukari ya Mtibwa na Kagera Ibrahim Ali ameishukuru TRA kwa kutoa semina elekezi na kuongeza kuwa elimu waliyoipata imewasaidia kuelewa mambo mengi kuhusiana na msamaha huo.

Msamaha wa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi unatokana na maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli aliyoyatoa katika Mkutano wa Baraza la Wafanyabiashara (TNBC) uliofanyika Ikulu tarehe 20 Machi, 2018 ambapo wafanyabiashara walilalamikia kuwepo kwa malimbikizo makubwa ya madeni ya kodi za nyuma yakijumuisha riba na adhabu.

Kufuatia maelekezo hayo, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilifanya marekebisho kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2018 na sehemu ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015 ambapo katika marekebisho hayo, Waziri wa Fedha na Mipango amepewa mamlaka ya kutoa utaratibu maalum wa kumuwezesha Kamishna Mkuu wa TRA kutoa msamaha wa riba na adhabu wa hadi asilimia 100 kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi tofauti na asilimia 50 ya hapo awali.

KAMATI KUU YA CCM YAJA NA MAAMUZI MAPYA


KAMATI Kuu Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) leo tarehe 14 Agosti, 2018 imeketi jijini Dar es Salaam na kufanya uteuzi wa wagombea watatu katika majimbo ya Monduli, Ukonga na Korogwe Vijijini.

Kamati hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dk. John Magufuli.

Kamati hiyo imemteua Julius Karanga kugombea jimbo la Monduli, Mwita Waitara ameteuliwa kugombea Ukonga na Timotheo Mzava ameteuliwa kugombea Korogwe Vijijini.

Katika hatua nyingine, kamati hiyo imewashukuru watanzania wote waliojitokeza kushiriki katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Buyungu na kata 77 na kukipa dhamana CCM na wagombea wake kwa kuwawezesha kushinda kwa asilimia mia.

TAKUKURU Hai Yamfikisha Mahakamani Mkuu wa Kitengo cha Uchaguzi na Mfanyabiashara Mmoja

Watu wawili akiwamo Mfanyabiashara wa mjini Moshi, Oscar Kigumu, wamefikishwa kortini jana Agosti 14, 2018 wilayanj Hai kwa tuhuma za ubadhirifu wa Sh27.6 milioni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Mfanyabiashara huyo anayemiliki kampuni ya Oscar Food and Beverage Catering Services, ameshitakiwa pamoja na mkuu wa kitengo cha uchaguzi wa Halmashauri ya Hai, Edward Ntakiliho.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 15, 2018




Mfumuko Wa Bei Wa Taifa Umepungua Kufikia Asilimia 3.3


Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Julai, 2018 umepungua hadi kufikia asilimia 3.3 ikilinganishwa na asilimia 3.4  mwezi Juni, 2018.

Hayo yameelezwa  jana na Jijini Dodoma na  Mkurugenzi wa sensa na Takwimu za Jamii, Ofisi ya Taifa ya Takwimu Ephraim Kwesigabo alipokuwa akitoa taarifa  ya mfumuko wa bei kwa mwezi Julai mwaka huu.

Kwesigabo alisema, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 imepungua ikilinganishwa na kasi ilivyokuwa kwa  mwaka ulioishia mwezi Juni, 2018.

“Kupungua kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 kumechangiwa hasa na kupungua kwa mfumuko wa bei wa baadhi ya bidhaa za vyakula, ambapo bidhaa za vyakula zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei kati ya Julai, 2017 na Julai 2018 ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 9.5, mtama kwa asilimia 17.8, unga wa mihogo kwa asilimia 14.1, matunda jamii ya machungwa kwa asilimia 22.2, maharagwe kwa asilimia 5.8 na mihogo mibichi kwa asilimia 12.5,” alifafanua Kwesigabo.

Aliendelea kusema kuwa ni zaidi ya miaka 15 tangu itokee tarakimu kama hiyo ya mfumuko wa bei ambayo iko vizuri kwa uchumi wa nchi.

Aidha alitaja hali ya mfumuko wa bei kwa baadhi ya  nchi za Afrika Mashariki kama ifuatavyo; Uganda mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 umeongezeka hadi asilimia 3.1 kutoka asilimia 2.2 kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018. Kwa upande wa Kenya mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Julai, 2018 umeongezeka hadi asilimia 4.35 kutoka asilimia kutoka asilimia 4.28 kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2018.

Mfumuko wa bei wa Taifa unapima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.

Rais Magufuli Ashindwa Kujizuia na Kumwaga Machozi Akimuaga Mzee Majuto


Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli ameshindwa kujizuia na kujikuta akimwaga machozi wakati alipokuwa akiaga mwili wa aliyekuwa msanii nguli wa vichekesho nchini, Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo Agosti 9, 2018.

Rais Magufuli alifika Karimjee na kujumuika na viongozi mbalimbali akiwemo Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete na waombolezaji wengine katika kuaga mwili wa nguli huyo aliyefariki dunia jana Jumatano, majira ya saa 2 usiku katika Hospitali ya Taifa Muhimbuili alipokuwa akitibiwa.

Mwili wa Mzee Majuto umesafirishwa kwenda nyumbani kwake jijini Tanga ambako atazikwa kesho Ijumaa, Agosti 10, 2018 mchana.

Kalanga, Waitara wapeta CCM

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kitafanya uteuzi wa wagombea ubunge katika majimbo ya Monduli, Korogwe na Ukonga Agosti 15 mwaka huu.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje, John Mrema amesema hayo leo Alhamisi Agosti 9.

“Wameanza kuchukua fomu za uteuzi ila sisi uteuzi ni Agosti 15, ndiyo vikao vitakaa na kuteua,” amesema Mrema.

Wakati chama hicho kikijipanga kufanya uteuzi huo, tayari Chama cha Mapinduzi (CCM), katika Jimbo la Monduli kimempitisha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo aliyejiuzulu wiki iliyopita, Julius Kalanga kuwa mgombea pekee licha ya wanaCCM Kuandamana kumpinga.

Kadhalika hali ikiwa hivyo katika Jimbo la Monduli, tayari aliyekuwa Mbunge wa Ukonga aliyejiuzulu na kuhamia CCM, Mwita Waitara anadaiwa kuchukua fomu kupitia chama hicho akiomba kuteuliwa kugombea tena jimbo hilo huku katika Jimbo la Korogwe wakitarajia kufanya uchaguzi leo.

Wiki iliyopita, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ilitangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika majimbo matatu na wa udiwani katika kata mbili za Tanzania Bara utakaofanyika Septemba 16, mwaka huu ambapo fomu za uteuzi wa wagombea wa majimbo hayo zitatolewa kuanzia Agosti 13 hadi 20, mwaka huu.

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top