Basi la Super Aljabir baada ya ajali.
watu 12
wamepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa baada ya Basi la Super
Aljabir linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Mahenge mkoani
Morogoro kugongana na treni maeneo ya Kiberege karibu na Ifakara,
Morogoro jioni hii.Ajali hiyo imetokea wakati basi hilo likijaribu kuwahi kuvuka reli kabla ya treni kupita.
Baadhi ya miili katika ajali hiyo ikiwa eneo la tukio.
********
WATU
12 wamefariki dunia papo hapo na wengine kadhaa wamejeruhiwa baada ya
basi walililkuwa wakisafiria la Kampuni ya Aljabir kugonga treni eneo la
Kiberege Ifakara Wilaya ya Kilombero.
Kamanda
wa polisi mkoani hapa Leonald Paulo alisema ajali hiyo ilitokea leo
majira ya saa 9:15 alasili baada ya basi hilo lilokuwa likitokea
Morogoro- Ifakara kugonga Treni ya Tazara iliyokuwa ikitokea Mbeya –
jijini Dar es Salaam.
Kamanda
huyo alisema kati ya watu hao sita wanaume, wanne wanawake na wawili
ni watoto wakike wenye umri kati ya miaka mitano na sita.
Kamanda
Paulo aliwataja marehemu watatu waliotambulika katika ajali hiyo kuwa
ni Frugensia Lusangila (60), Albeta Lusangila (62) wakazi wa Ichonde
Mangula na Joseph Kazwila (34) mkazi wa jijini Dar es Salaam.
Kamanda
Paulo alisema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa basi hilo lenye namba
za usajili T725 ATD Scania, alivuka barabara yenye makutano na reli
bila ya kuchukua tahadhani na hivyo kuigonga treni.
Alisema
kuwa majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika hospitali ya mtakatifu
Fransis Ifakara na kituo cha afya Kibaoni kwa ajili ya matibabu.
Kamanda Paulo alisema miili ya marehemu nayo imehifadhiwa katika hospitali ya mtakatifu Frances Ifakara.
Alisema
dereva wa basi hilo alikimbia mara baada ya ajali hiyo kutokea na
polisi wanamtafuta wakati uchunguzi ukiwa bado unaendelea.
on Friday, November 7, 2014








Post a Comment