ANGELO ENRIQUE AKIWA NA JEZI YAKE MPYA YA MANCHESTER UNITED
ANGELO ENRIQUE AKISAINI MKATABA WA MANCHESTER UNITED PEMBENI YAKE NI SIR ALEX FERGUSON
AKIWA OLDTRAFFORD
Hatimaye
Manchester united imethibitisha kumsajili mchezaji mwenye umri wa miaka
18 Angelo Enriquez kutoka katika klabu ya universidad de chile ya
nchini chile .
Mchezaji huyo kutoka chile
amekamilisha vipimo vya afya na kutua rasmi katika klabu ya manchester
united kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 4.
Mchezaji huyo ambaye alikuwa
anakipiga katika klabu ya universidad de chile alifanikiwa kufunga
magoli 11 katika michezo 17 aliyoichezea klabu yake ya zamani katika
msimu uliopita na kuweza kuisaidia timu yake kunyakua taji la ligi hiyo.
Akimwongelea mchezaji huyo kocha
wa manchester united sir alex ferguson amesema mchezaji huyo ni hazina
kubwa kutokana na kasi na uwezo wake mkubwa wa kuweza kuusoma mchezo
awapo uwanjani, ni mchezaji wa aina yake kwa umri mdogo alionao
.
Tuna
sifa ya kuendeleza vipaji vya wachezaji chipukizi na angelo anafaa
kuingia katika rekodi za manchester united kutokana na uwezo wake
alionao.
Akiongea na mtandao wa
manchester united mchezaji huyo amesema anajisikia furaha kuwa mahali
hapo na kuendelea kusisitiza kwamba manchester united ni timu kubwa
duniani na inaongozwa na kocha bora kabisa duniani.
Manchester united imethibitisha mchezaji huyo atakuwa anavaa jezi namba 21
Post a Comment