|  | 
| Uganda, mabingwa wa kihistoria wa Challenge | 
NA 
MAHMOUD ZUBEIRY
MICHUANO ya 
soka ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama CECAFA 
Challenge Cup, mwaka huu itafanyika mjini Kampala, Uganda kuanzia Novemba 24 
hadi Desemba 8.
Kampuni ya 
Bia Afrika Mashariki (EABL), kupitia bia yake ya Tusker Lager, ndio wadhamini 
michuano hiyo kwa dau lao la dola za Kimarekani 450,000 walizitoa kwa ajili ya 
michuano ya mwaka huu ya Kombe la CECAFA –Tusker Challenge 
Cup.
Katibu wa 
CECAFA, Nicholas Musonye alisema mapema tu wakati wa maandalizi ya awali ya 
michuano hiyo, kwamba lengo la michuano hiyo ni kuzisaidia maandalizi timu za 
Afrika Mashariki na Kati katika kuwania tiekti ya kucheza Fainali za Kombe la 
Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.
Udhamini wa 
mwaka huu huo ni ongezeko la aslimia 5, kutoka michuano ya mwaka jana mjini Dar 
es Salaam, ambayo Uganda waliibuka mabingwa.
Ni udhamini 
ambao utahusu usafiri, malazi na huduma nyingine, wakati jumla ya dola za 
Kimarekani 60.000 zitakuwa kwa ajili ya zawadi, bingwa akipewa dola 30.000, 
mshindi wa pili dola 20.000 na dola 10.000 mshindi wa tatu.   Kama ilivyo ada, 
mechi zote za michuano hiyo zitaonyeshwa na Televisheni ya Super Sport ya Afrika 
Kusini.
Michuano 
hiyo huandaliwa na CECAFA, Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati, 
ambalo lina wanachama 12.
Japokuwa 
ukanda wa CECAFA ndiyo eneo linalojikongoja kwa sasa katika soka ya kimataifa, 
lakini ukweli ni kwamba, mpira wa miguu barani Afrika, ulianzia ukanda wa Afrika 
Mashariki.
Michuano ya 
kwanza kabisa mikubwa barani Afrika, ilihusisha mataifa manne, 
Kenya , Uganda , Tanganyika  (sasa Tanzania Bara) na Zanzibar 
Michuano 
hiyo ya Gossage ambayo sasa imekuwa Kombe la Challenge, ilifanyika mara 37 
kuanzia mwaka 1926 hadi 1966, ilipobadilishwa jana na kuwa michuano ya wakubwa 
ya soka kwa mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, ilifanyika mara saba kati ya 
mwaka 1965 na 1971, ilipozaliwa rasmi CECAFA Challenge.
Michuano 
hiyo ilikuwa ikidhaminiwa na bepari aliyekuwa akimiliki kiwanda cha sabuni, 
William Gossage, aliyezaliwa Mei 12 mwaka 1799 na kufariki dunia Aprili 9, mwaka 
1877.
Michuano 
hiyo mikongwe zaidi barani, imekuwa ikiandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka 
Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), ikihusisha timu za taifa za ukanda 
huo.
Hadi 
inafikia tamati michuano ya Gossage , 
Uganda  ilikuwa inaongoza kwa 
kutwaa taji hilo , mara 22, ikifuatiwa na 
Kenya  iliyotwaa mara 12 na 
Tanzania 
Mwaka 2005, 
michuano hiyo ilifanyika chini ya udhamini wa bilionea wa Ethiopia mwenye asili 
ya Saudi Arabia, Sheikh Mohammed Al Amoudi na kupewa jina la Al Amoudi Senior 
Challenge Cup, lakini sasa Tusker ndiyo mambo yote.
MABINGWA 
CHALLENGE;
Mwaka 
Bingwa          
1973    
Uganda 
1974    
Tanzania 
1975    
Kenya 
1976    
Uganda      
1977    
Uganda 
1978    
Malawi 
1979    
Malawi 
1980    
Sudan 
1981    
Kenya 
1982    
Kenya 
1983    
Kenya 
1984    
Zambia 
1985    
Zimbabwe 
1986   
Haikufanyika
1987    
Ethiopia 
1988    
Malawi 
1989    
Uganda 
1990    
Uganda 
1991    
Zambia 
1992    
Uganda 
1993   
Haikufanyika 
1994    
Tanzania 
1995    
Zanzibar 
1996    
Uganda 
1997   
Haikufanyika 
1998   
Haikufanyika     
1999    
Rwanda 
2000    
Uganda 
2001    
Ethiopia 
2002    
Kenya 
2003    
Uganda 
2004    
Ethiopia 
2005    
Ethiopia 
2006    
Zambia 
2007    
Sudan 
2009    
Uganda 
2009    
Uganda 
2010    
Tanzania Bara
2011    
Uganda
KUNDI A: 
Uganda, Kenya, Ethiopia na Sudan Kusini
KUNDI 
B: Tanzania, Sudan, Burundi na Somalia
KUNDI 
C: Malawi, Eritrea, Rwanda na Zanzibar
RATIB KUNDI 
A:
Novemba 24, 
2012: 
Ethiopia v 
Sudan               (Saa 9:00 Alasiri) 
Uganda v 
Kenya                (Saa 12:00 jioni)
Novemba 27, 
2012: 
Sudan Kusini 
v Kenya       (Saa 9:00 Alasiri) 
Uganda v 
Ethiopia             (Saa 12:00 jioni)
Novemba 30, 
2012: 
Kenya v 
Ethiopia               (Saa 9:00 Alasiri) 
Sudan Kusini 
v Uganda     (Saa 12:00 jioni)
RATIBA KUNDI 
B:
Novemba 25, 
2012: 
Burundi v 
Somalia             (Saa 9:00 Alasiri) 
Tanzania v 
Sudan              (Saa 12:00 jioni)
Novemba 28, 
2012: 
Somalia v 
Sudan                (Saa 9:00 Alasiri) 
Tanzania v 
Burundi           (Saa 12:00 jioni)
Desemba 1, 
2012: 
Sudan v 
Burundi                (Saa 9:00 Alasiri) 
Somalia v 
Tanzania           (Saa 12:00 jioni)
RATIBA KUNDI 
C:
Novemba 26, 
2012: 
Zanzibar v 
Eritrea             (Saa 9:00 Alasiri) 
Rwanda v 
Malawi             (Saa 12:00 jioni)
Novemba 29, 
2012: 
Malawi v 
Eritrea               (Saa 9:00 Alasiri) 
Rwanda v 
Zanzibar           (Saa 12:00 jioni)
Desemba 1, 
2012: 
Malawi v 
Zanzibar            (Saa 9:00 Alasiri) 
Eritrea v 
Rwanda              (Saa 12:00 jioni)
ROBO 
FAINALI:
Desemba 
3, 2012 
Mshindi 
Kundi C vs Mshindi wa Pili Kundi B (Saa 10:00 
jioni)
Mshindi 
Kundi A vs Mshindi wa Tatu Bora wa pili (Saa 1:00 
usiku)
Desemba 
4, 2012 (16:00): 
Mshindi 
Kundi B vs Mshindi wa Tatu Bora wa kwanza (Saa 10:00 
jioni)
Mshindi wa 
Pili Kundi A vs Mshindi wa Pili Kundi C       (Saa 1:00 
usiku)
NUSU 
FAINALI: 
Desemba 6, 
2012
Nusu Fainali 
ya Kwanza    (Saa 10:00 jioni) 
Nusu Fainali 
ya Pili           (Saa 1:00 usiku)
MSHINDI WA 
TATU: 
Desemba 
8, 2012 
Waliofungwa 
Nusu Fanali (Saa 10:00 jioni)
FAINALI: 
Desemba 
8, 2012
Walioshinda 
Nusu Fainali  (Saa 1:00 usiku)
WASIFU WA TIMU ZINAZOSHIRIKI TUSKER CHALLENGE 2012
|  | 
| Kenya | 
NYOTA WA 
HARAMBEE:
|  | 
| Sudan | 
MWEWE WA 
JANGWANI;
TIMU ya 
taifa ya Sudan inajulikana kwa jina la utani kama Sokoor Al-Jediane Kiarabu, 
Kiingereza Desert Hawks, yaani Mwewe wa Jangwani. Hii ilikuwa moja ya nchi tatu 
tu nyingine zikiwa ni Misri na Ethiopia zilizoasisi Kombe la Mataifa Huru ya 
Afrika mwaka 1957 na ilifanikiwa kushinda taji hilo mwaka 1970, wakiwa wenyeji, 
baada ya kuwafunga Ghana 1-0 kwenye fainali, wakitoka kuifunga Misri 2-1 katika 
Nusu Fainali. Sudan ni miongoni mwa timu kongwe barani Afrika na ilikuwa ina 
historia ya utajiri miaka ya 1950 na 1970. Sudan pia ilishika nafasi ya pili 
kwenye michuano hiyo katika fainali za mwaka 1959 zilizofanyika mjini Cairo, 
Misri zikishirikisha nchi tatu, yani mbali na wenyeji, pia walikuwapo Ethiopia. 
Ilishika tena nafasi ya pili katika fainali za mwaka 1963 baada ya kufungwa na 
Ghana 
|  | 
| Uganda | 
KORONGO WA 
KAMPALA; 
Uganda 
ambayo timu yake ya taifa inaitwa The Cranes, yaani Korongo hawajawahi kufuzu 
kwenye fainali za Kombe la Dunia, na kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya 
Afrika matokeo yao mazuri kabisa ni kushika nafasi ya pili mwaka 1978, baada ya 
kufungwa na wenyeji Ghana 2-0 mjini Accra. Lakini Korongo wa Uganda wanajivunia 
kuwa timu iliyotwaa mara nyingi zaidi taji (mara 12) Kombe la Challenge, katika 
miaka ya 1973, 1976, 1977, 1989, 1990, 1992, 1996, 2000, 2003, 2008, 2009 na 
2011 na pia imeshika nafasi ya pili mara nne.
|  | 
| Rwanda | 
NYIGU WA 
KIGALI;
| Burundi | 
MBAYUWAYU WA 
BUJUMBURA;
Lakini ni 
nchi ambayo imebarikiwa wachezaji wenye vipaji, ingawa wengi baadaye huikana 
nchi hiyo na kuchukua uraia wa nchi jirani, kwa mfano Nonda Shabani aliyehamia 
DRC na Hamadi Ndikumana aliyejivika Unyarwanda. 
|  | 
| Somalia | 
MABAHARIA WA 
MOGADISHU;
|  | 
| Zanzibar | 
MASHUJAA WA 
VISIWANI;
Zanzibar pia 
imewahi kuingia Nusu Fainali mara sita na mbili ikishika nafasi ya tatu, wakati 
michuano ya mwaka huu, inaeonekana kuwa na kikosi imara zaidi. 
|  | 
| Ethiopia | 
SWALA 
DUME;
Ethiopia 
ambayo timu yake ya taifa inajulikana kama The Walya Antelopes, mchanganyiko wa 
maneno mawili, la Kiingereza na Kihabeshi, lenye maana ya ‘Swala dume’ ni 
miongoni mwa nchi tatu pamoja na Misri na Sudan zilizoasisi michuano ya Mataifa 
Huru ya Afrika mwaka 1957 na wakafanikiwa kutwaa taji hilo mwaka 1962 walipokuwa 
wenyeji, ingawa baada ya muongo huo, ilipoteza makali yake. 
Baada ya 
kuzisakosa kidogo fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2004, kwa kuzidiwa pointi 
tatu tu, baada ya kufungwa na Guinea, Ethiopia mwakani itashiriki tena fainali 
hizo nchini Afrika Kusini, baada ya miaka 31. Inajivunia pia kutwaa mataji ya 
Challenge katika miaka ya 1987, 2001, 2004 na 2005.
|  | 
| Tanzania Bara | 
NYOTA WA 
KILIMANJARO;
Haijawahi 
kushiriki fainali hata moja za Kombe la Dunia, lakini inajivunia kucheza fainali 
moja za mwaka 1980 za Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Nigeria, sambamba na 
kutwaa mara tatu Kombe la Challenge katika miaka ya 1974, 1994 na 2010 na 
kushika nafasi ya pili mara tano. 
| Malawi | 
MWALE WA 
NYASA;
Mafanikio 
yao 
|  | 
| Sudan Kusini | 
NYOTA ANGAVU 
WA SUDAN KUSINI;
Sudan 
Kusini, au Bright Star, yaani Nyota Angavu kwa jina la utani, huyu ni mwanachama 
mpya kabisa wa CECAFA, nchi iliyojigawa kutoka Sudan ambayo sasa inatambulika 
katika familia ya soka kama taifa kamili. Kwao hizi zitakuwa fainali za kwanza 
kabisa za Challenge. Sudan Kusini rasmi ilicheza mechi yake ya kwanza ya 
kimataifa Julai 10, mwaka huu na kutoka sare ya 2-2 na Uganda nyumbani. Hii ni 
kuashiria kwamba, pamoja na upya wao si timu ya kubeza kwa kitendo cha kutoka 
nguvu sawa na mabingwa watetezi wa michuano hii.
|  | 
| Eritrea | 
WAVUVI WA 
BAHARI NYEKUNDU ERITREA;
Imekosekana 
katika fainali mbili zilizopita za Challenge kutokana na tabia ya wachezaji wake 
kuzamia nchi za watu wanapokwenda kucheza mechi. Wachezaji wanne wa klabu ya Red 
Sea FC walizamia Nairobi baada ya mechi ya Ligi ya Mabingwa na wengine 12 wa 
timu ya taifa wakazamia Tanzania mwaka 2007 baada ya Challenge. Wachezaji 
wengine sita walizamia Angola Machi mwaka 2007 baada ya mechi ya kufuzu ya Kombe 
la Mataifa ya Afrika. Wachezaji wengine watatu zaidi walizamia Sudan, hivyo 
Eritrea ikajitoa kwenye soka ya kimataifa kwa ujumla ili kutafuta dawa ya 
kukabiliana na tatizo hilo na sasa serikali ya nchi hiyo inamtaka kila mchezjai 
kuweka nakfa 100,000 (fedha za kwao) kabla ya kusafiri nje. Timu yao ya taifa 
inaitwa Red Sea Boys, yaani vijana wa Bahari Nyekundu na haina cha kujivunia 
kwenye mashindano haya, ikiwa ilicheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa Juni 
26, mwaka 1992 na kutoka 1-1 na Sudan.
VIWANGO VYA 
UBORA FIFA
NCHI              
NAFASI
Uganda            
86
Malawi            
101
Ethiopia           
102
Sudan              
102
Rwanda           
122
Burundi           
128
Kenya              
130
Tanzania          
134
Zanzibar          
134
Somalia           
193
Eritrea             
192
Sudan 
Kusini   200
(Viwango 
hivi vimetoka mwezi huu)

 


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment