Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SHUGHULI ZA UOKOZI ZASITISHWA GHANA




Shughuli za uokozi zilivyoendelea

Juhudi za uokozi katika jengo la ghorofa lililoporomoka wiki jana nchini Ghana zimesitishwa.
Kwa mujibu wa maafisa waliokuwa wanasimamia shughuli hiyo, mjini Accra, idadi ya watu waliofariki imefika 14, wala sio kumi na nane kama ilivyoripotiwa hapo awali huku watu wnegine 67 wakinusurika.

Mmiliki wa jengo hilo, pamoja na afisaa anayesimamia ubora wa majengo, wamezuiliwa.Ujenzi mbovu umelaumiwa kwa kuanguka kwa jengo hilo lenye maduka na amblo lilifungua rasmi mapema mwaka huu.
Rais John Dramani Mahama, alisema kuwa wale waliohusika na kupuuza usalama na ubora wa jengo hilo lazima watachukuliwa hatua kali.
'manusura wangali hospitalini'
Msemaji wa jeshi, kanali, M'bawine Atintande alisema siku ya Jumapili kuwa waokoaji waliweza kufika eneo la chini ya jumba hilo na kwamba hawakuwa na matumaini ya kupata manusura zaidi.
Takriban watu 81 waliokolewa kutoka chini ya vifusi, kumi na wanne kati yao wakiwa wamefariki alisema kanali bila ya kuelezea kwa nini waokoaji walikuwa wamekadiria wale waliofariki kuwa 18.
Kati ya manusura 67 waliopelekwa hospitalini, 13 wangali wanapokea matibabu huku 54 wakiruhusiwa kwenda nyumbani.
Afisaa mmoja alihojiwa na kisha kuachiliwa kwa dhamana.
Mnamo siku ya Alhamisi, idara ya uhandisi nchini humo, ilisema kuwa jengo hilo halikuwa na kibali kumaanisha kuwa huenda halikukaguliwa kabla ya kufunguliwa rasmi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top