Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TAARIFA ZA MAREJESHO YA KODI KUFANYIKA KWA NJIA YA MTANDAO

 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeanzisha utaratibu wa kuwasilisha taarifa za marejesho ya kodi kwa njia ya mtandao kwa lengo la kuboresha na kurahisisha uwasilishaji wa taarifa hizo.


Kaimu Mkurugenzi wa TRA, Allan Kiula, aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuwa lengo la kuanzisha utaratibu huo ni kuwapa fursa walipakodi kuhifadhi taarifa zao katika kopyuta kwa ajili ya kumbukumbu zao na kurahisisha uhakiki wa taarifa zinazotumwa.


Alisema lengo lingine ni kupunguza uwapo wa makosa kwenye taarifa zinazotumwa na kuondoa msongamano kwenye ofisi za mamlaka ya mapato.


Kiula alisema kupitia utaratibu huo, walipa kodi watawasilisha taarifa za marejesho ya kodi zao wakiwa mahali popote pale, hususan majumbani au ofisini.


Alisema watakaokuwa wanatuma taarifa kwa njia ya mtanadao, ni wale, ambao watakuwa wamejisajili pekee na dole gumba.


Aliwataka ambao hawajajisajili, kujisajili ili waweze kutumia utaratibu huo.

habari NA ELIZABETH ZAYA
CHANZO: NIPASHE
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top