Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

USAFIRI WA TRENI DAR WA MWAKYEMBE UNAVYOWATESA WANAFUNZI

 
Baadhi ya wanafunzi wanaosafiri kwa treni kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam kuelekea Ubungo wakiwa wamepanga mabegi yao kwenye mstari huku wao wakiwa wamepumzika pembeni wakisubiri usafiri huo. Kwa utaratibu wa kawaida wa usafiri huo abiria hutakiwa kupanga foleni ili inapowasili kila abiria aingie kadri ya ulivyowahi kwenye foleni hiyo.
Baadhi ya wanafunzi wanaosafiri kwa treni kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam kuelekea Ubungo wakiwa wamepanga mabegi yao kwenye mstari huku wao wakiwa wamepumzika pembeni wakisubiri usafiri huo. Kwa utaratibu wa kawaida wa usafiri huo abiria hutakiwa kupanga foleni ili inapowasili kila abiria aingie kadri ya ulivyowahi kwenye foleni hiyo.


BAADHI ya Wanafunzi jijini Dar es Salaam ambao hutumia treni ya abiria inayofanya safari zake Ubungo na Katikati ya Jiji la Dar es Salaam (Stesheni) wamebudi staili mpya ya kuepuka kupanga mstari mrefu huku wakisimama muda mrefu kusubiri usafiri huo.


Wanafunzio hao wanapofika mapema kituoni hupanga mabegi yao kwa mstari na wao kupumzika pembeni hadi treni inapofika ndipo huinuka katika maeneo mbalimbali waliokaa na kuingia kwenye mstari kwa kufuata begi la mtu. Begi moja kwenye mstari humwakilisha mwanafunzi mmoja. Thehabari imeshuhudia utaratibu huu waliobuni wanafunzi kuepuka wao kusimama muda mrefu wakiisubiri treni kuwasili kituoni.


Kikawaida abiria wanaosafiri kwa treni hiyo wakiwemo wanafunzi husimama kwa foleni kwa muda mrefu wakisubiri usafiri huo, huku kukiwa hakuna viti vya kutosha kupumzikia wasafiri wanaposubiri usafiri huo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top