Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WENZA WA VIONGOZI WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUKEMEA UVUNJAJI WA MAADILI NCHINI

Wenza wa viongozi yaani mke au mume, viongozi wa dini na watoto wenye umri chini ya miaka 18 wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kukemea uvunjaji wa maadili nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome Kaganda alipokuwa akizungumza wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Tovuti ya Sekretarieti hiyo.
Kamishna huyo alisema wenza wa viongozi wanayo nafasi kubwa ya kukemea uvunjaji wa maadili pale anapomuona mwenzake anafanya hivyo ili kuhakikisha wanafuata maadili yanayostahili.
Kamishna huyo pia amewaomba viongozi wa dini nao wasaidie kukemea vitendo vya ukosefu wa maadili kwa waumini wao. Aliongeza kuwa kama kuna desturi ya kuungama dhambi basi viongozi wa dini wawakumbushe waumini wao kufanya hivyo.
Akizungumzia watoto wenye umri wa chini ya miaka 18 ambao sheria ya Maadili pia inawagusa, Kamishna Kaganda alisema wanayo nafasi kubwa ya kuwakumbusha kwa heshima na bila kuwakosea adabu wazazi wao wajibu wao na kuwaeleza wazi kwamba Cheo ni dhamana wasikichezee ili kuwalinda.
Alisema suala la ukosefu wa maadili katika makundi mbalimbali ya jamii limekuwa ni janga la kitaifa hivyo aliwataka watanzania kurudi kwenye Utamaduni wa Kitanzania.
Kamishna Kaganda alisema fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni pia zitapatikana kwenye tovuti iliyozinduliwa leo na kwamba hivi sasa zimeshasambazwa kwa viongozi wote wa Umma, na wanatakiwa kuzijaza na kurejesha kabla au ifikapo Disemba 31 mwaka huu kwa ajili ya kufanyiwa kazi.
Alisema kiongozi yeyote atakayekiuka Agizo hilo la serikali atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya mwaka 1995. Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa sheria hiyo kifungu (i), kiongozi anapaswa kujaza fomu hizo katika siku 30 baada ya kupewa wadhifa wake, kila mwisho wa mwaka wa kalenda na mwisho wa kutumikia wadhifa au cheo chake.
Akizindua Tovuti hiyo, Naibu Katibu Mkuu- Ikulu Bibi Susan Mlawi alisema Tovuti hii ni muhimu kwa kuwa itarahisisha upatikanaji wa huduma na habari mbalimbali kwa lengo la kuelimisha Umma pamoja na kuwajengea wananchi uwezo wa kupata taarifa muhimu kupitia teknolojia ya Habari na mawasiliano yaani TEHAMA.
Alisema Tovuti aliyoizindua pia itawawezesha viongozi wa Umma nchini kote kupata na kujaza Fomu za Tamko la Rasilimali na Madeni na hivyo kuziwasilisha Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa wakati.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top