Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kesi ya viongozi wa Uamsho Zanzibar yatupwa


 
MAHAKAMA Kuu ya Zanzibar ,imetupilia mbali kesi ya viongozi wa Uamsho waliokuwa wanadai kunyimwa huduma muhimu wakiwa mahabusu.
Jaji Mkusa Isaack Sepetu jana aliitupa kesi hiyo namba 2 ya mwaka 2012 iliyokuwa imefunguliwa dhidi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, Ibrahim Mzee Ibrahim.
Jaji Sepetu alisema kesi hiyo iliyofunguliwa na mawakili Abdallah Juma Mohammed, ilifunguliwa kinyume na kifungu cha 4 sura ya 28 cha Sheria za Mawakili na Wanasheria wa a Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).
Alisema pamoja na mambo mengine, nyaraka zimekosa, jina la mtu aliyekula kiapo kwa niaba ya washtakiwa nalo halipo.
Alisema kimsingi mambo hayo hayakukidhi hoja za kisheria kwa hivyo anaitupa kesi hiyo iliyofunguliwa na viongozi wa Uamsho. Viongozi wa Uamsho walifungua kesi hiyo wakidai kwamba hawatendewi haki katika Mahabusu ya Kiinua Miguu, iliyopo Zanzibar, kwa kunyimwa haki za kubadilisha nguo, kuabudu, kuonana na jamaa zao na zingine.
Wakili wa washtakiwa hao, Salum Toufioq alisema kwamba wateja wake sasa wanapewa huduma hizo lakini hawajaruhusiwa kuonana na jamaza zao tangu kesi hiyo ilipoanza.
Jaji Mkussa alisema kwa mujibu wa sheria ya vyuo vya mafunzo Zanzibar, washtakiwa wana haki ya kupewa huduma zote sawa na mahabusu wengine.
Kesi ya msingi inayowakabili viongozi hao itaendelea Januari 3, mwakani.
Viongozi hao ni Masheikh Farid Hadi Ahmed, Msellem Ali Msellem, Azzan Khalid Hamdan, Mussa Juma Issa, Suleiman Juma Suleiman, Khamis Ali Suleiman na Hassan Bakari Suleiman.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top