Naomba kuchukua fursa 
hii kutoa shukrani za dhati na wazi kwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania, Mheshimiwa 
Jakaya Kikwete na Serikali yake ya awamu ya nne, kwa niaba yangu binafsi na kwa 
niaba yaTawi la CCM UK na nina imani kwa niaba ya wana jamii ya Wa-Tanzania 
Walioko Nje ya Nchi (Dispora)  kwa Ujumla, katika juhudi anazofanya kujumuisha 
Dispora Tanzania kwenye kuchangia maendeleao ya Nchi yetu. 
Wana-Dispora tulio wengi 
tumeshuhudia kwa vitendo 
tangu Rais Jakaya 
Kikwete na Serikali yake imeingia Madarakani , jitihada  na mikakati tofauti na 
iliyo wazi  ya Serikali Kuu  kutafuta mbinu za kudumu ili kushirikiana na 
kuwahusisha wana Diaspora, katika kuchangia maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii ya 
Nyumbani, Tanzania.
Nakumbuka Mheshimiwa 
Rais Kikwete katika kikao chake cha kwanza na Watanzania waishio Uingereza Mnamo 
mwaka wa fedha 2006/2007  pale Churchill Hotel, UK , katika Hotuba yake ambayo 
mbali na kutuelezea mafanikio na mikakati mbalimbali iliyopangwa na serikali 
yake kwenye utekelezaji wa Sera zake za Serikali ya awamu ya nne, kwa nia ya 
 kutimiza maazimio ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005 na baadae 2010, vile vile 
alituahidi wana-Dispora kuwa atahakikisha yeye Binafsi atafanya jitihada zake 
zote kwa kadri ya uwezo wake aliyopewa na Mwenyezi Mungu  na Serikali yake 
haitusahau na katuacha nyuma Wana-Dispora . Kilichoendelea baada ya Mkutano ule 
wana Dispora UK tulishudia thamani yetu kwa Serikali na Taifa letu ,kwani 
tumekuwa tukipewa kipaumbele kwa kila Kiongozi Mkuu wakiwemo Mawaziri na Wabunge 
wetu tofauti,  wanapotembelea  Uingereza (na nina imani Nchi nyingine mbalimbali 
) mbali na kuwa na ratiba zao ndefu za  kikazi, wanapata  muda wa kubadilishana 
mawazo nasi na tunaona matunda ya mchango wetu yameanza kuonekana ,licha ya 
kuwepo changamoto za kawaida zinazokabilika.  Hili  tunamshukuru sana Rais wetu 
kwa kulipa uzito unaostahili na kuonyesha mfano wa Uongozi wake bora na 
uliotukuka.
Kwa mara ya kwanza 
Tanzania Dispora  tumepata sauti na kuthaminiwa kwa wazi kwa Mchango wetu wa 
hali na  mali tunaorudisha nyumbani ili kuchangia Maendeleo ya Nchi. 
Wana-Dispora sasa  tunajivunia kupewa  na  Rais wetu  jina la Mkoa . Baada ya 
kuanza na dawati la Dispora pale Wizara ya Mambo ya Nje, ili kuweka mfumo wa 
kudumu na kutimiza ahadi yake Mheshimiwa Rais mwaka ulipita 2012 aliteua 
Mkurugenzi wa Idara ya Dispora. Sasa tuna Idara/Kitengo kizima na si dawati 
tena. Kitengo/Idara yenye jukumu la kushughulikia mambo muhimu na tofauti ya 
Dispora. Hii ni hatua kubwa sana na ya muhimu na hatutaacha kumshukuru Rais wetu 
kwa kuliona na kulitambua hili na kutuletea matunda yake. 
Licha ya yote hayo ya 
kiutendaji yanayoendelea, na jambo kubwa lililofanya kuandika shukrani hizi za 
dhati na za wazi ni kilichotendeka wiki iliyopita kupitia vyombo vya habari na 
Blogu za jamii tumeshuhudia tukio la kihistoria pale ambapo Rais Jakaya Kikwete, 
Chini ya Ofisi yake Ikulu , wametoa fursa kwa Wa-Tanzania Wataalamu waliopo Nje 
na Ndani ya Nchi kupeleka  wasifu wao (CV) moja kwa moja Ofisi za Katibu Mkuu 
Kiongozi -Ikulu,   ili tuweze kupata nafasi za kazi kuchangia moja kwa moja na 
kuwa mstari wa mbele kuijenga nchi yetu . Hiki kimekuwa kilio cha muda mrefu cha 
Watanzania (na hususan Wana-Dispora) kuomba serikali kutumia zaidi wataalamu wa 
kitanzania na si wa kigeni , na  tumefurahi sana kuwa Serikali yetu kwa mara ya 
kwanza na kwa uwazi kabisa  imetusikiliza kwa hili . 
Naomba kutoa wito na 
shime kwa WaTanzania wote waliopo nchi mbalimbali  duniani  , ni wakati umefika 
sasa Nchi yetu inatuhitaji na Serikali yetu imetupa nafasi hii adhimu basi na 
tujipange na tujitokeze kwa wingi ili tuweze kwenda nyumbani kuchangia maendeleo 
ya Tanzania yetu katika nyanja tofauti na kwa kadri ya uwezo wetu na kwa yale 
mazuri tuliyojifunza Ughaibuni.  
 naomba kumalizia kwa 
ule usemi usemao kuwa "Asiyemshukuru Binadamu mwenzie basi hata Mwenyezi Mungu 
hawezi kumshukuru " na kwa mantiki hiyo, kwa heshima kubwa Naomba kutanguliza 
shukrani zangu za dhati  kwa mpendwa Rais wetu Jakaya Mrisho Kikwete kwa 
kujitolea kwake na kufanya kazi ngumu mno ya kuliongoza Taifa letu na 
nakumuombea kwa Mwenyezi Mungu yeye  Binafsi na Viongozi wetu wote afya njema na 
hekima za kuweza kupambana na majukumu yao ya kila siku .
Kwa Wana -Dispora 
Wenzangu popote pale mlipo Duniani , ngoma iko uwanjani na tuicheze sasa, CV 
zinahitajika .........haya mama  Harambeeeee 
Mugu Ibariki Afrika, 
Mungu Ibariki Tanzania 
Umoja Ni Ushindi 
.
Kidumu Chama Cha 
Mapinduzi. 
Mariam 
Mungula 
Katibu wa CCM - 
Uingereza 

 


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment