Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TUSKER YAIBEBA SIMBA NUSU FAINALI MAPINDUZI CUP

Tusker ya Kenya, imekuwa timu ya kwanza kufuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, baada ya jioni hii kuilaza Jamhuri ya Pemba bao 1-0, lililofungwa na mshambuliaji wake hatari, Jesse Were dakika ya 23 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Mabingwa hao wa Kenya, sasa wamefikisha pointi saba na kujiimarisha kileleni mwa Kundi A na kwa matokeo hayo, Simba SC pia tayari imefuzu Nusu Fainali, kwani mabingwa hao wa Bara tayari wana pointi nne hadi sasa, wakati Jamhuri imemaliza na tatu na Bandari haina pointi hata moja. Simba inacheza mechi ya mwisho na Bandari usiku Amaan.

source: Bin Zubeiry
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top