Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAMA SALMA KATIKA SHEREHE ZA MIAKA 36 YA CCM MKOANI LINDI

IMG_6755Mama Salma Kikwete akihutubia mamia ya wananchi wa mkoa wa Lindi waliohudhuria sharehe za kutimiza miaka 36 ya Chama cha Mapinduzi zilizofanyika kimkoa katika kijiji cha Rondo kata ya Chiponda mkoani Lindi tarehe 5.2.2013.

IMG_6468Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akifungua rasmi jengo la CCM Tawi la Rondo kata ya Chiponda huko Lindi Vijijini wakati wa kilele cha sherehe ya kutimiza miaka 36 ya CCM zilizofanyika kimkoa kijijii hapo tarehe 5.2.2013. Kulia kwa Mama Salma ni Mjumbe wa NEC Taifa, Mbunge wa Mtama na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Bernard Membe.
IMG_6475Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akifurahia mara baada ya kulifungua rasmi jengo la CCM Tawi la Rondo kata ya Chiponda huko Lindi Vijijini wakati wa kilele cha sherehe ya kutimiza miaka 36 ya CCM zilizofanyika kimkoa kijijii hapo tarehe 5.2.2013. Kulia kwa Mama Salma ni Mjumbe wa NEC Taifa, Mbunge wa Mtama na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Bernard Membe.
IMG_6544Ngoma ya Linyamwa ya kabila la Wamwera ikichezwa na wananchi wa kijiji cha Mpenda kutoka wilaya ya Lindi vijijini wakati wa kilele cha sherehe ya kutimiza miaka 36 ya kuzaliwa Chama Cha Mapinduzi zilizoazimishwa kimkoa katika kijiji cha Rondo tarehe 5.2.2013.
IMG_6572Mama Salma Kikwete aliyekuwa mgeni rasmi katika sherehe za kutimiza miaka 36 ya CCM Mkoani Lindi akijumuika na wacheza ngoma ya Linyamwa kucheza ngoma hiyo. Sherehe hizo zilifanyika katika kijiji cha Rondo huko Lindi vijijini tarehe 5.2.2013.
IMG_6685Mjumbe wa NEC na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mheshimiwa Bernard Membe akimvisha skafu Bwana Omary Issa kutoka Chama cha Wananchi, CUF, akiwa ni miongoni mwa wanachama wapya waliojiunga na CCM kutoka vyama vingine vya siasa wakati wa kilele cha sherehe za kutimiza miaka 36 ya kuzaliwa chama hicho.
IMG_6702Mjumbe wa NEC Taifa kutoka wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akimkabidhi kadi ya CCM mwanachama mpya ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja wakati wa sherehe za kutimiza miaka 36 ya chama hicho zilizofanyika kimkoa katika kijiji cha Rondo huko Lindi Vijini tarehe 5.2.2013,
IMG_6746Baadhi ya wananchi wakisikiliza kwa makini hotuba kutoka kwa mgeni rasmi Mama Salma Kikwete wakati wa kilele cha kutimiza miaka 36 ya ChamaCha Mapinduzi. Sherehe zilizofanyika kimkoa katika kijiji cha Rondo kata ya Chiponda huko Lindi vijijini tarehe 5.2.2013.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top