Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MBUNGE WA CCM OLE SENDEKA AHOJIWA

 

MBUNGE wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na vigogo kadhaa wa CCM Wilaya ya Simanjiro Mkoa wa Manyara, wamehojiwa na maofisa wa CCM, kuhusiana na malalamiko ya ukiukwaji wa taratibu katika uchaguzi wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa ya chama hicho (Nec) wa wilaya hiyo.


Hatua hiyo ni utekelezaji wa mikakati ya Makamu Mwenyekiti wa CCM (Tanzania Bara), Phillip Mangula, ambaye aliahidi kushughulikia malalamiko yote ya chaguzi zilizopita na kuyatolea uamuzi. Mangula ndiye Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Maadili ya CCM.


Kuhojiwa kwa Sendeka na viongozi wengine wa Simanjiro, kumekuja siku chache baada ya kuhojiwa kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk Mary Nagu ambaye pia ushindi wake wa Nec Wilaya ya Hanang, ulilalamikiwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye akisema kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu na kanuni za uchaguzi wakati wa kinyang’anyiro hicho.


Katika uchaguzi wa Simanjiro, Sendeka alishinda kwa kupata kura 471 dhidi ya Diwani wa CCM Kata ya Mirerani, Justin Nyari ambaye alipata kura 126.





Maofisa hao kutoka Makao Makuu ya CCM, wakiongozwa na Mwanasheria wa CCM, Glorius Luoga waliwahoji Sendeka na Katibu wa CCM Wilaya ya Simanjiro, Jamillah Mujungu, Nyari na viongozi wengine wa chama hicho.




Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika wikiendi iliyopita, zimebainisha kuwa Nyari na makada kadhaa wa CCM, wanalalamikia ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi huo, ikiwamo kufanyika kwa kampeni kinyume cha taratibu kama kutawaliwa na ukabila, pia baadhi ya wapigakura kutokuwa halali.




Hata hivyo, Luoga ambaye pia ni Mjumbe wa Nec anayetoka Songea Vijijini, alipotakiwa kuelezea hatma ya malalamiko hayo, hakutaka kufafanua kwa maelezo kuwa yupo Zanzibar.
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Manyara, Ndekubali Ndeng’aso alikiri kufika kwa maofisa wa makao makuu ya chama hicho mkoani hapo na kuhojiana na walalamikaji na walilalamikiwa.




“Nadhani hizi ni taratibu za kawaida tu ndani ya chama, kuna ambao wamelalamika sasa chama kimeona ni busara kuwafuata na kujua malalamiko yao,” alisema Ndeng’aso.
Sendeka na Nyari hawakupatikana jana kuelezea kilichojiri katika mahojiano hayo kwani simu zao za mkononi ziliita bila ya kupokewa.




Hata hivyo, Mujungu licha ya kukiri kuhojiwa alisema wenye mamlaka ya kuzungumza ni maofisa hao wa makao makuu... “Hili jambo lipo ngazi za juu nadhani wao ndiyo wana majibu ya maswali yenu.”
Mwananchi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top