Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Serikali yatakiwa kufuta suala la uzoefu wa ajira

MBUNGE wa Iramba Magharibi Mwigulu Nchemba (CCM) jana aliibana Serikali na kuitaka itamke kufuta suala la uzoefu kwa watu wanaoomba ajira mpya.
Nchemba alitoa kauli hiyo katika swali lake kwa Waziri Mkuu ambapo alisema Tanzania hakuna chuo kinachofundisha masuala ya uzoefu kazini.
Mbunge huyo ambaye ni Naibu Katibu Mkuu (CCM) Bara, alielezwa kukerwa kwake na kitendo cha utitiri wa viongozi wanaokaimu nafasi zaidi ya mbili ilhali wapo vijana ambao hawana kazi.
“Mheshimiwa Waziri Mkuu, taasisi za Serikali zimekuwa na utaratibu wa kuwataka watu wanaoomba ajira wawe na uzoefu wakati kuna upungufu mkubwa wa watumishi mpaka Tume ya Mipango, wakati huohuo wasiokuwa na kazi ni wengi ni kwa nini suala la uzoefu linakuwa ni kikwazo?” alihoji Nchemba.
Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikiri kuwa ni kweli Tanzania kuna upungufu mkubwa wa watumishi na hasa kada ya ualimu na afya.
Alisema kuwa Serikali inatumia taratibu mbalimbali kwa ajili ya kumaliza matatizo ya upungufu wa watumishi ukiwamo kuajiri wapya huku akisema kuwa upungufu wa walimu utakuwa ni mgumu kuisha mapema kutokana ongezeko kubwa la wanafunzi kwa sasa.
Wakati huohuo, Serikali inakusudia kupeleka bungeni muswada wa sheria ili kuifanyia marekebisho sheria iliyotungwa kuhusu Hifadhi na Ngorongoro.
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye alisema kuwa kilio cha wenyeji wa Ngorongoro ni cha msingi na hivyo kinapaswa kusikilizwa.
Alisema hayo alipokuwa akijibu swali la papo kwa hapo kutoka kwa Mbunge wa Viti Maalumu Nameok Sokoine ambaye alihoji taratibu zinazochukuliwa na Serikali katika kulishughulikia tatizo la wananchi wa Ngorongoro ambao wanakabiliwa kwa kiasi kikubwa na njaa.
Sokoine alisema Serikali haikuwatendea haki wananchi wa Ngorongoro kwa kubadilisha matumizi ya ardhi yao bila ya kuwashirikisha licha ya kuwa wameishi katika maeneo hayo hata kabla ya ukoloni.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top