Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UKOSEFU WA UTAALAMU CHANZO CHA KUONNGEZEKA KWA MAKOSA YA JINAI


 

images


IMEELEZWA kuwa ukosefu wa utaalamu wa kutosha katika eneo la urejeshaji wa mali zilizopatikana kwa njia haramu ndicho chanzo cha kumomonyoka kwa maadili na ongezeko la vitendo vya makosa ya jinai katika jamii.
Hayo yalisemwa leo (jana) na Mkurugenzi wa Mashtaka(wakati akifungua mafunzo ya kuijengea nchi uwezo wa urejeshaji wa mali zilizopatikana kwa njia haramu yanayoendelea katika ukumbi wa mikutano wa jengo la Haki House, jijini Dares Salaam.
“Wahalifu wamekuwa kukiendelea kufanya vitendo hivi na kufahia matunda yake, kwa sababu wapelelezi waendesha mashtaka na maofisa wa mahakama kutokuwa na utaalamu kwenye eneo la urejeshaji wa mali zilizopatika kwa njia haramu. Ofisi yangu imewaalika wataalamu kutoka World Bank/ StAR intiative kwa ajili ya kutoa ushauri na mbinu za kuweza kukabiliana na changamoto hii,alisema Feleshi.

Alisema maafunzo hayo yamewashirikisha wadau mbalimbali kutoka Benki ya Kuu ya Tanzania (BOT), Financial Interligent Unit,Polisi,Wizara ya Malia Asili, Usalama wa Taifa na Wakala wa Usajili wa Leseni za Kampuni (BRELA).
Aidha Feleshi alisema mafunzo hayo yatakamilika Februari 27, mwaka huu yatasaidia kuwapa wadau hao uzoefu kutoka nchi ya Afrika Kusini, ambayo imeonekana kufanya vizuri. Pia wadau hao watapata ujuzi jinsi taasisi hiyo inavyofanya kazi .
Feleshi alisema mafunzo hayo yatawasaidia wadau hao kuona namna ya kuweza kufanya kazi kwa pamoja ili kudhibiti tatizo la wahalifu kufanya vitendo hivyo,lakini mali zao hazirejeshi serikali au kwa wahusika.
Alisema ofisi yake ilianzisha kitengo hicho mwaka 2009, imeshaanza kulifanyia kazi suala hilo, hivyo mhalifu anapofanya uhalifu anachunguzwa na mali zake huchunguzwa ili kuona zimepatikana vipi huku akitolea mfano wa meli ya uvuvi ya Kichina ambayo ilitaifishwa na kurejesha serikalini
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top