Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kufuatia kushuka kwa kiwango cha ufaulu kidato cha nne 2012 Serikali yaandaa Mkakati wa Kuboresha Matokeo (Better Results Now -BRN).

 

Mwenyekiti wa Tume ya kuchunguza kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa kidato cha nne 2012 Profesa Sifuni Mchome.
 
Tume ya kuchunguza chanzo cha kushuka kwa kiwango cha ufaulu wa mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, imesema Serikali inaandaa mkakati wa kuboresha matokeo unaojulikana kama Mkakati wa Kuboresha Matokeo (Better Results Now -BRN).
Mwenyekiti wa Tume hiyo Profesa Sifuni Mchome amesema lengo la mkakati huo ni kuleta maendeleo ya elimu nchini na tayari wataalamu wa ndani na nje ya nchi wanashiriki kikamilifu katika kufanikishwa zoezi hilo
Profesa Mchome amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizugumza na waandishi wa habari juu ya hatua iliyofikiwa mpaka sasa na Tume hiyo katika kutekeleza majukumu yake ya uchunguzi na kupata majibu kutoka kwa wadau wa elimu nchini.

Mwenyekiti huyo amewaomba wananchi, taasisi mbalimbali na hata vyama vya siasa nchini bila kujali itikadi zao, kushiriki na kuhamasishana katika utoaji wa maoni kwa tume ili kufanikisha utatuzi wa changamoto zinazokwaza maendeleo ya elimu nchini.
Profesa Mchome amesema pamoja na changamoto za muda mrefu zinazoikabili sekta ya elimu nchini, taifa bado linaendelea kupiga hatua na kujiwekea dhamira na mikakati ya kuleta maendeleo kupitia sekta mbalimbali.
Amefafanua kuwa changamoto hizo zinahitaji kuwekewa nguvu za pamoja na kutoa maoni endelevu ili kupata mustakabali wa jinsi ya kuinua elimu nchini katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu.
Profesa Mchome amesema hadi sasa wamefanya mahojiano na taasisi, mamlaka na wadau mbalimbali wa elimu nchini ambao wameainisha sababu za kushuka kwa kiwango cha ufaulu katika mtihani huo.
Ametaja baadhi ya taasisi na mamlaka hizo kuwa ni Chama cha Wamiliki wa Shule Binafsi nchini (TAMONGSCO), Chama cha Walimu Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) kanda ya Dar es Salaam, Chama cha Walimu Tanzania, viongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Taasisi ya Elimu Tanzania na Baraza la Mitihani Tanzania.
Wadau wengine waliohojiwa na tume hiyo ni Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala, Mameya, Maafisa Elimu wa miko ya Dar es Salaam na Tanga, Wakaguzi wa Elimu, Wajumbe na Wakuu wa shule mbalimbali za Dar es Salaam, wazazi wanafunzi na wananchi kwa ujumla.
“Mpaka sasa tumeshapokea ujumbe mfupi wa simu zaidi ya 300, ujumbe kupitia tume tumepokea zaidi ya 200, baruapepe nyingi sana na watu tuliokutana nao ni zaidi ya 40, pia tumepokea simu nyingi sana ingawa changamoto ni mazungumzo” amesema Profesa Mchome na kuongeza kuwa:
“Maoni tuliyoyapata mpaka sasa ni shida ya walimu hawatoshi, uchache wa vitabu, hali ya majengo hairidhishi na umbali wa shule, na hizi shida zipo kwenye shule za Serikali na binafsi na kuna baadhi ya shule binafsi ni nzuri lakini zina shida zaidi”
Kwa sasa wajumbe wa tume wako katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Manyara, Arusha, Morogoro, Pwani, Simiyu, Shinyanga na Mbeya ambapo wanafanya mahojiano na wakuu wa mikoa na wilaya na shule, walimu, wanafunzi na wajumbe wa bodi za shuke za sekondari zilizoko kwenye mikoa hiyo.
Mwenyekiti huyo amesema baada ya wajumbe wa tume hiyo kumaliza kazi katika mikoa hiyo, watafanya safari za Zanzibar na Dodoma kuanzia Mchi 24 na kufanya mahojiano na viongozi wa serikali wa visiwa vya Unguja na Pemba na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Tume ya kuchunguza chanzo cha kushuka kwa kiwango cha ufaulu wa mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, iliundwa na Waziri Mkuu Machi 2 mwaka huu ili kutafua sababu zilizochangia matokeo yasiyoridhisha ya mtihani huo na inatarajiwa kukamilisha kazi yake baada ya majuma manne kuanzia sasa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top