MENEJA wa Wafanyakazi wa Ndani ya Ndege wa Kampuni ya
Fastjet Emma Donovan, alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Dar es
Salaam kujibu shtaka linalomkabili la kutoa lugha ya matusi.
Emma (40) alipandishwa kizimbani jana na kusomewa
shtaka hilo na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga, mbele ya Hakimu Joyce
Minde.
Katuga alidai Machi 19 mwaka huu Emma alimtolea lugha ya matusi Samson Itinde jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Emma alikana shtaka hilo ambapo Katuga alidai upelelezi umekamilika na kuomba kupangiwa tarehe kwa usikilizwaji wa awali.
Katuga alidai Machi 19 mwaka huu Emma alimtolea lugha ya matusi Samson Itinde jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Emma alikana shtaka hilo ambapo Katuga alidai upelelezi umekamilika na kuomba kupangiwa tarehe kwa usikilizwaji wa awali.
Hakimu Joyce alisema kuwa dhamana ya mshtakiwa iko wazi
lakini kwa kuzingatia vigezo vya dhamana vitakavyotolewa kwa kuwa mshtakiwa ni
raia wa kigeni.
Alitaja masharti ya dhamana kuwa mshtakiwa anatakiwa
kuwasilisha hati yake ya kusafiria au kutoa fedha taslim sh milioni tano na pia
awe na wadhamini wawili ambao ni Watanzania.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 9 ili kupangwa
tarehe ya kuanza kwa usikilizwaji wa awali.



1 comments:
tanzania needs to get over the use of words like shit and fuck!!! you see it all the time on the radio here and on tv, grow up!!!
ReplyPost a Comment