Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI WAMPA WAKATI MGUMU WAZIRI SITTA

 


Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta

Na: Beatrice Moses
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewajibu wabunge wa Afrika Mashariki akisema wengi hawahudhurii vikao vya kupewa mwongozo kuhusu bunge hilo kwa kuwa “wanataka kulipwa posho”. Kauli hiyo ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, imekuja siku moja tangu wabunge hao waichongee wizara hiyo kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, kwamba imeshindwa kuwapa mwongozo pale wanapokwenda kwenye vikao vya Bunge la Afrika Mashariki. Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo jana, Sitta alisema wabunge hao wamekuwa vinara wa kuomba posho kila
wanapotakiwa kuhudhuria kwenye mikutano ya wizara yake.
Katika maelezo yake Sitta alimeshutumu Katibu wa Wabunge hao, Shyrose Bhanji kuwa ndiye anayeongoza kwa kutoa udhuru mara kadhaa, hivyo kutoudhuria vikao vinavyoitishwa na wizara hiyo.
“ Wizara imejiwekea utaratibu mzuri wa kukutana na wabunge hao, lakini nafikiri katibu wao ndiye anayeongoza kwa kutohudhuria,” alisema Sitta na kuongeza:

“Nadhani amekuwa na shughuli nyingi sana, tuna utaratibu wa kukutana kila baada ya miezi mitatu, lakini ndiye aliyeongoza pia kutoa malalamiko hayo yasiyo na ukweli.”
Waziri Sitta katika majibu yake alifafanua kwamba wizara hiyo bado haijapewa majukumu rasmi ya kutoa mwongozo kwa wabunge hao.
Mbali na Sitta, naibu wake, Abdullah Juma Saddallah naye alieleza tabia za wabunge hao huku akisisitiza kuwa posho kwao ndiyo jambo la umuhimu zaidi.
Saddallah alisema malalamiko hayo ni ya ajabu na yamewashtua kwa sababu hayana ukweli, lakini wamekuwa wakijikuta kwenye mtihani kwani kuna baadhi ya wabunge hao wakiitwa kuudhuria vikao utambulia kuuliza posho.
“Wizara haina fungu la kuwahudumia wabunge hao, hili limekiwishajadiliwa katika vikao vya kamati vilivyopita na ilikubalika kuwa ofisi ya bunge itaangalia uwezekano wa kuwapatia ofisi na vitendea kazi vingine,” alisema Saddallah.
Alisema pia kabla ya kuteuliwa wabunge hao wizara hiyo kwa kushirikiana na ofisi ya Bunge ilifanya uchambuzi na kuandaa mwongozo utakaowezesha ushirikiano na uwajibikaji baina ya Bunge la Tanzania na wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).
“Mwongozo huu umewezesha kuundwa kwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambayo awali ilitarajiwa kuwa Kamati ya Bunge ya Afrika Mashariki inayotoa nafasi ya kutoa taarifa za utekelezaji na kupata mwongozo,” alisema Naibu Waziri huyo.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top