Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MKUU WA WILAYA YA KAHAMA BENSON MPESYA ALITAKA JESHI LA POLISI KUWAKAMATA WATU WALIOMUUWA SAJENTI SALIM NDANI YA WIKI MOJA.



MKUU WA WILAYA YA KAHAMA BENSON MPESYA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WALIOHUDHURIA KATIKA MSIBA HUO.
MAREHEMU SALIM MTEPA ENZI ZA UHAI WAKE
MWILI WA MAREFEMU SALIM MTEPA UKIWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KAHAMA MUDA MCHACHE BAADA YA KUFARIKI.

KAHAMA
Mkuu wa wilaya ya Kahama Mh.Benson Mpesya ameliagiza jeshi la Polisi wilayani humo kuhakikisha ndani ya wiki moja wanawatia mbaroni watu waliofanya mauaji ya Sajenti Salim Mtepa (41) usiku wa kuamkia leo.

Agizo hilo amelitoa leo wakati akitoa salamu za pole nyumbani kwa marehemu ambapo mwili wa marehemu ulikuwa ukiagwa kabla ya safari ya kuelekea jijini Dar es salaam.

Sambamba na hayo amewataka vijana wilayani kahama kutafuta pesa kwa njia zilizo halali na kuacha kutafuta pesa kwa njia za mkato ikiwemo wizi,ukabaji na utapeli.

Katika hatua nyingine amewataka vijana wasiokuwa na ajira mjini kurudi vijijini kwao ili kujishughulisha na kilimo wakiwasaidia wazazi wao badala ya kukaa vijiweni na kujiingiza katika makundi mabaya.

Kwa upande wake Mkuu wa kituo cha Polisi wilayani Kahama George Simba amemwambia mkuu wa wilaya kuwa tayari zoezi la kuwasaka watu hao limeanza na kuongeza kuwa lazima watu hao wapatikane.

Naye Kaimu kamanda mkuu wa Mkoa Wa Shinyanga Onesmo Lyanga amesema kuwa damu ya Sajenti Salim haiwezi kwenda bure na kwamba watahakikisha jeshi la Polisi linawatia mbaroni watuhumiwa hao.

Pamoja na hayo ametoa wito kwa Wananchi wilayani kahama kutoa taarifa za siri endapo watapata tetesi zozote kuhusu tukio hilo.
 
kb blog
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top