Wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida imetangaza ‘operation ondoa tembe’baada ya matukio ya wakazi wake kuendelea kupoteza maisha kutokana na kuangukiwa na nyumba za tembe. Wilaya hiyo mpya imeagiza kila mkazi awe na nyumba bora kama njia mojawapo ya kukomesha vifo vinavyotokana na kuangukiwa na nyumba za tembe.(Picha na Nathaniel Limu).

Na Nathaniel Limu
Mvua ya kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani Singida zimesababisha watu wanne wakazi wa wilaya ya Mkalama na mifugo 14 ya aina mbalimbali kufariki dunia baada kuangukiwa na nyumba za tembe.