Katibu wa Halmashauri Kuu ya
CCM Taifa, (Itikadi na Uenezi), Nape Nnauye amesema Chadema ni chama
kilichovamiwa na watu wanaotumia siasa kuganga njaa.Nape alisema hayo jana
wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM,
Abdulrahman Kinana
“Ndugu zangu kuweni
macho kwa sasa, siasa imeingiliwa na watu wasiokuwa na sifa za uongozi na kazi
yao kubwa ni kutumia siasa kuganga njaa zao,” alisema.
Alisema wananchi
wanapaswa kuwa macho na wanasiasa
hao ambao malengo
yao ni kuwaangamiza wananchi.
Akitaja baadhi ya
sifa za wanasiasa aliowaita makanjanja, Nape alisema wengi wao ndiyo wanaotaka
madaraka kwa gharama yoyote.
Alisema
Chadema wanachojua kwa sasa ni kuwahujumu wale wote wenye mawazo tofauti na yao
kwa kuwatesa na hata kupoteza maisha ya wanaowapinga.
“Badala ya kushindana kwa
hoja na sera, wanachokijua wao ni kung’oa kucha za wanaowapinga, kuwatesa na
wakati mwingine hata kumwaga damu kwenye operesheni zao,”
alisema.
Alisema kwa kuwa wamekusudia
kwa gharama yoyote kushika dola, hawajali damu za Watanzania zinazomwagika ili
mradi wanafanikisha wanalolitaka.Akikumbushia operesheni mbalimbali zilizofanywa
na Chadema nchini tangu uchaguzi uishe mwaka 2010, Nape alitoa mifano ya
operesheni ya mjini Arusha, Morogoro, Iringa, Singida na kwingine ambako maisha
ya baadhi ya Watanzania yalipotea lakini hawakushtuka wala
kuwajibika.
“Tunamwamini Mungu hataruhusu
damu hizi ziendelee kumwagika kisa wanasiasa makanjanja, pia laana ya damu hizi
zilizomwagika zitaviua vyama hivi na nchi yetu itabaki salama,”
alisema.
Nape
alitoa wito kwa wananchi kuwa macho dhidi ya wanasiasa wa namna
hiyo.
“Hewa wanayovuta wanasiasa makanjanja ni ya watu
wanaowaunga mkono, tunaweza kuamua leo kuwanyima hewa hiyo na huo ndiyo utakuwa
mwisho wao,”alisema Nape.
SOURCE::MWANANCH
Katibu wa Halmashauri Kuu ya
CCM Taifa, (Itikadi na Uenezi), Nape Nnauye amesema Chadema ni chama
kilichovamiwa na watu wanaotumia siasa kuganga njaa.Nape alisema hayo jana
wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM,
Abdulrahman Kinana
“Ndugu zangu kuweni
macho kwa sasa, siasa imeingiliwa na watu wasiokuwa na sifa za uongozi na kazi
yao kubwa ni kutumia siasa kuganga njaa zao,” alisema.
Alisema wananchi
wanapaswa kuwa macho na wanasiasa
hao ambao malengo
yao ni kuwaangamiza wananchi.
Akitaja baadhi ya
sifa za wanasiasa aliowaita makanjanja, Nape alisema wengi wao ndiyo wanaotaka
madaraka kwa gharama yoyote.
Alisema
Chadema wanachojua kwa sasa ni kuwahujumu wale wote wenye mawazo tofauti na yao
kwa kuwatesa na hata kupoteza maisha ya wanaowapinga.
“Badala ya kushindana kwa
hoja na sera, wanachokijua wao ni kung’oa kucha za wanaowapinga, kuwatesa na
wakati mwingine hata kumwaga damu kwenye operesheni zao,”
alisema.
Alisema kwa kuwa wamekusudia
kwa gharama yoyote kushika dola, hawajali damu za Watanzania zinazomwagika ili
mradi wanafanikisha wanalolitaka.Akikumbushia operesheni mbalimbali zilizofanywa
na Chadema nchini tangu uchaguzi uishe mwaka 2010, Nape alitoa mifano ya
operesheni ya mjini Arusha, Morogoro, Iringa, Singida na kwingine ambako maisha
ya baadhi ya Watanzania yalipotea lakini hawakushtuka wala
kuwajibika.
“Tunamwamini Mungu hataruhusu
damu hizi ziendelee kumwagika kisa wanasiasa makanjanja, pia laana ya damu hizi
zilizomwagika zitaviua vyama hivi na nchi yetu itabaki salama,”
alisema.
Nape
alitoa wito kwa wananchi kuwa macho dhidi ya wanasiasa wa namna
hiyo.
“Hewa wanayovuta wanasiasa makanjanja ni ya watu
wanaowaunga mkono, tunaweza kuamua leo kuwanyima hewa hiyo na huo ndiyo utakuwa
mwisho wao,”alisema Nape.
SOURCE::MWANANCH
Post a Comment