MAJASUSI  wa shirikisho la ujasusi la 
nchini Marekani wamefika jijini Arusha kusaidiana na wapelelezi wa nchini 
Tanzania katika uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa bomu  kwa 
waumini wa kanisa katoliki na Balozi wa Vatican nchini siku ya 
jumapili. 
Magesa alitoa taarifa hiyo wakati akitoa taarifa ya 
Mkoa kwa waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda alipozuru 
eneo la tukio na kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika hospitali mbalimbali na 
kuwapa pole.
Wakati maafisa hao wakifika jijini humo tayari vyombo 
vya usalama vinawashikilia watu zaidi ya 10 miongoni mwao wakiwemo watu wanne 
 kutoka Saudia Arabia ambao waliwasili nchini kupitia uwanja wa 
ndege wa Kilimanjaro(KIA) siku moja kabla ya tukio.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo alisema kuwa watu 
hao walikamatwa muda mfupi wakiondoka  nchini kupitia mpaka wa 
Namanga kuelekea nchini  Kenya baada ya tukio kutokea.
Hata hivyo taarifa hiyo haikuweza kutoa ufafanuzi zaidi 
na kwamba taarifa zaidi juu ya upepelezi zitatolewa kadri muda na wakati 
utakavyoruhusu.



Post a Comment