Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Spika wa Bunge atembelea majeruhi wa Mlipuko uliotokea mjini Arusha na kutoa rambirambi iliyotolewa na wahe. Wabunge kwa baba askofu wa Jimbo kuu la Arusha Askofu Josephat Lebulu

 

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akipokewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Magesa Mulongo katika Uwanja wa Ndege wa KIA.
Askofu Mkuu wa jimbo kuu la Arusha Baba Askofu Josephat Lebulu akizungumza jambo na Spika wa Bunge,Mh. Anne Makinda juu tukio lililotokea hivi karibuni.
Paroko Pedy Kasterino wa paroko ya Tokeo la Bwana Bulka Olasite akimpa maelezo Mhe. spika jinsi mlipuko ulivyotokea katika kanisa la Mt. Joseph Olasite Mjini Arusha.



Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwafariji katika majeruhi katika Hospitali ya Mount Meru kufuatia Mlipuko uliotokea katika Kanisa la Mt. Joseph Olasite, Mjini Arusha na kusababisha Vifo vya watu 3 kufariki na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa jumapili iliyopita.
Paroko Pedy Kasterino wa paroko ya Tokeo la Bwana Bulka Olasite akimuongoza Mhe. Spika kuangalia eneo mlipuko huo ulipotokea.
Spika wa Bunge akiwapa pole wananchi waliofika eneo la parokia ya Mt. Joseph Olasite alipofanya ziara ya kutembelea eneo ambalo mlipuko ulitokea jumapili.
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini, Mhe. John Mongela akimkaribisha Mhe. Spika pamoja na ujumbe wa Wabunge alioambatana nao katika Uwanja wa KIA.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Magesa Mulonga akitoa taarifa kwa Mhe. Spika pamoja na Wabunge jinsi tukio la mlipuko ulivyotokea katika parokia ya Mt. Joseph Olasite Mjini Arusha Jumapili iliyopita.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Mhe. Capt. George Mkuchika , Mhe. Pindi Chana na Mhe. Richard Ndasa wakimsikiliza kwa Makini Mkuu wa Mkoa.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiushukuru Mkoa wa Arusha kwa juhudi zilizofanya mpaka sasa katika kuwasaka wahalifu waliotekeleza shambulio hilo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimpa pole Askofu Mkuu wa jimbo kuu la Arusha Baba Askofu Josephat  Lebulu kutokana na Mlipuko uliotokea jumapili iliyopita katika Parokia ya Mt. Joseph Olasite.
Baba askofu akisalimiana na waheshimiwa wabunge.
Spika wa Bunge pamoja na wabunge wakimfariji baba askofu pamoja na uongozi wa Kanisa Katoliki Tanzania.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwasilisha rambirambi zilizotolewa na wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa Askofu wa jimbo kuu la Arusha Baba Askofu Josephat  Lebulu kufuatia mlipuko ulisababisha vifo vya watu 3 jumapili iliyopita na kuacha watu zaidi ya 60 majeruhi.
Picha zote na Owen Mwandumbya

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top