Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TAWI LA CCM DMV LINATOA SALAMU ZA POLE KWA WATANZANIA WALIO ATHIRIKA ARUSHA

 




TAWI LA CCM WASHINGTON DC, MARYLAND& VIRGINIA

Chama cha Mapinduzi tawi la Washington DC, Maryland na Virginia, tumesikitishwa na tukio la mlipuko siku ya Jumapili, Mei 5 2013 mjini Arusha.

Chama cha Mapinduzi tawi la DMV tuna laani vikali shambulio hilo lililofanywa na mtu au watu katili, waovu na wenye dhamira mbaya kwa Taifa letu la Tanzania. Tukio hilo la kusikitisha limepoteza mtanzania mwenzetu na kusababisha wengine 40 kupata majeraha na maumivu makali.

Tunaamini serikali itafanya kazi yake ya kuwasaka wahusika na wote walioshiriki kufikishwa kwenye mkono wa sheria.

Tunatoa rambi rambi kwa watanzania wenzetu walioathirika kwa kuondokewa na wapendwa wao na wale wote waliopatwa na majeraha katika tukio hilo. Mwenyezi mungu awape nafuu ili warejee kwenye shughuli zao za kila siku.

Mungu ibariki Tanzania


UONGOZI WA TAWI LA CCM
WASHIGTON DC, MARYLAND NA VIRGINIAMAREKANI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top