Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BEI ZA MAFUTA ZAPUNGUA .... VIWANGO VYA BEI MPYA HIVI HAPA

BEI za mafuta ya dizeli, petroli na mafuta ya taa zimepungua kwa tofauti ya sh 16 na 72 kwa lita ikilinganishwa na mwezi uliopita.

Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam juzi na Injinia Mutaekulwa Mutegeki wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) ilisema kila mwezi mamlaka hiyo imekuwa ikitangaza bei kikomo na elekezi ili kudhibiti upandaji holela wa bei kwa mafuta.

Ilibainisha kuwa bei hizo zimeanza kutumika jana na mafuta ya petroli yamepungua sh 16 kwa lita sawa na asilimia 0.76; dizeli sh 42 sawa na asilimia 2.16 na mafuta ya taa kwa sh 72 sawa na asilimia 3.50.

Taarifa hiyo ilibainisha bei za bidhaa za mafuta zitaendelea kupangwa na soko, huku Ewura itashiriki kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta.

Iliongeza kuwa mabadiliko hayo ya bei yametokana na bei za mafuta katika soko la dunia sambamba na sheria ya mafuta ya mwaka 2008.

Taarifa hiyo iliweka wazi kuwa kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani ilimradi ziko chini ya bei kikomo kama ilivyokokotolewa na kanunimpya iliyopitishwa na Ewura mwaka 2011 .

Wakati huo huo, vituo vyote vya mafuta vimetakiwa kuchapisha na kuonyesha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana yakionyesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika.

Mkurugenzi huyo mkuu aliwatahadharisha wamiliki wa vituo vya mafuta kuwa ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja na adhabu itatolewa kwa kituo husika.

TANZANIA DAIMA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top