MKE wa naibu wa chifu 
katika wilaya ya Marigat Alhamisi aliaga dunia katika hali isioeleweka baada ya 
mumewe kumpata akinywa pombe haramu ya chang’aa katika nyumba ya 
jirani.
Naibu wa chifu wa kata ya 
Arabal Bw William Yegon inasemekana hakufurahia pale alipompata mkewe Bi Mary 
Kobilo, 46, akipiga mtindi na wanakijiji wengine.
Wenyeji walioongea na 
Taifa Leo walisema kuwa wawili hao walianza kuzozana wakati wa tukio hilo la saa 
kumi na mbili jioni Jumatano huku naibu huyo wa chifu akimlaumu mkewe kwa 
kumwaibisha kwa kunywa pombe hiyo haramu ilhali yeye alikuwa afisa wa serikali 
anayefaa kuongoza vita dhidi ya pombe haramu.
“Naibu huyo wa chifu alikasirishwa sana kwamba mkewe alikuwa 
akimkosea heshima licha ya serikali kutangaza vita kwa wapikaji wa pombe 
haramu,”alisema mmoja wa wanakijiji ambao hakutaka kutajwa 
jina.
Alisema kuwa baada ya 
ugomvi huo marehemu alipepesuka nje ya nyumba lakini hakwenda nyumbani kwake. 
Mwili wake ulipatikana katika msitu mmoja karibu na kwake Alhamisi 
mchana.
Akithibitisha tukio 
hilo,mkuu wa wilaya ya Marigat Bw Saul Moywaywa alisema kuwa uchunguzi tayari 
umeanzishwa kubaini kiini cha kifo cha mwanamke huyo.
Sumu
“Mwili wake haukuwa na 
alama yoyote. Tunashuku alijitoa uhai wake kwa kumeza sumu,”Bw Moywaywa 
aliambia Taifa Leo kwa njia ya simu.
Mwili wa marehemu 
ulichukuliwa na kupelekwa katika hifadhi ya maiti ya hospitali ya wilaya ya 
Kabarnet kusubiri upasuaji

 


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment