SHIRIKISHO
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawashukuru washabiki kwa kujitokeza
kwa wingi kwenye mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Taifa Stars
na Ivory Coast (The Elephants) iliyochezwa juzi (Jumapili) kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam.
Mwitikio
wa washabiki katika mechi hiyo ilikuwa ni moja ya chachu ya kiwango
kilichoonyeshwa na Taifa Stars, kwani walishangilia mwanzo hadi mwisho
licha ya kupoteza kwa mabao 4-2.
Ni
matarajio utakuwepo mwitikio kama huo huo katika mechi ijayo ya Taifa
Stars ya michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Nyumbani (CHAN)
dhidi ya Uganda (The Cranes) itakayochezwa Dar es Salaam kati ya Julai
12-14 mwaka huu. Stars itaingia tena kambini Julai 4 mwaka huu kujiandaa
kwa mechi hiyo.
Post a Comment