Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UKUMBI WA STEREO KINONDONI WATEKETEA KWA MOTO MCHANA WA LEO .... ONA PICHA ZA WAKATI LIKIUNGUA NA BAADA YA KUUNGUA

 Gari la zimamoto likiwa eneo la tukio likizima moto ulioteketeza Ukumbi wa Stereo leo mchana. Mashuhuda wa liokuwepo eneo hilo walisema kuwa Mtoto huo ulioanza majira ya saa nane mchana umeelezwa kuwa umetokana na hitirafu ya umeme iliyoanza baada ya kutokea cheche za moto wakati mmoja wa wapambaji alipokuwa akiendele na kazi ya kupamba ukumbi huo kwa ajili ya sherehe iliyokuwa ifanyike ukumbini hapo leo jioni. 

Mashuhuda wengine walitonya kuwa baada ya moto huo Mtungi wa gesi uliokuwa jikoni pia uliripuka na kuongeza kasi ya moto huo. Aidha imeelezwa kuwa baada ya moto huo, gari la zimamoto liliwasili eneo la tukio baada ya dakika 20 ulipotokea moto huo lakini, liliondoka bila kufanya kazi hiyo ya kuzima moto baada ya kufika eneo hilo na kujikuta halina maji na hivyo likaondoka kwenda kujaza maji na kurejea tena.
 Hapa ni kwenye kona ya ukumbi huo kama inavyoonekana.
 Mamia ya wananchi wakishuhudia moto huo ukiteketeza ukumbi huo.
 Mmoja kati ya waliojitokeza kusaidia kuzima moto huo akimwaga maji ndani ya ukumbi huo kumalizia kuzima moto huo. Kwa picha zaidi bofya hapa chini

 Akizima moto wa mwisho mwisho......
 Majirani waliosaidia kuzima na kuhamisha vitu katika nyumba hii iliyo jirani na ukumbi huo.
 Majirani waliowahi kuhamisha vitu vyao vya ndani kabla ya moto huo kuanza kusambaa katika nyumba nyingine, kwani moto huo umesambaa katika nyumba tatu za jirani na eneo hilo, lakini uliwahi kuzimwa.
 Majirani wakiwa nje ya nyumba zao....
 Kijana wa Zimamoto akitandaza mpira wa maji ili kupitisha maji kuelekea kwenye moto huo.
 Jinsi moto huo ulivyoteketeza vifaa vyote ikiwa ni pamoja na viti vilivyokuwa vikiandaliwa kwa ajili ya sherehe iliyokuwa ifanyike jioni ya leo ukumbini hapo.
 Baadhi ya vijana wakijisevia mabaki...
 Na wale wa vyuma chakavu hawakuwa mbali, hapa wakikusanya mabaki ya vyuma....
 Gari la zimamoto likiendelea kuzima moto huo.
 Taswira ya ajali hiyo ya moto.
Sehemu ya wananchi wakiendelea kushangaa.






Bar maarufu Kinondoni iitwayo 'STEREO' imateketea kwa moto mkubwa sana jioni ya leo. Moto huo unadhaniwa ulitokana hitilafu ya umeme katika bar hiyo. Pamoja na bar hiyo kuteketea pia nyumba tatu  lilizokuwa jirani na bar hiyo pia zimeathirika na mali nyingi kuharibika. 
 
Credits: Sufiani Mafoto & Jestina George Blogs
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top