Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAJASIRIAMALI SASA KUPUMUA, UFUMBUZI WA CHANGAMOTO ZAO WAPATIKANA

 


2CHANGAMOTO zinazowakabili wajasiriamali wadogo katika utunzaji wa kumbukumbu na kuwafanya wasiaminike, kupatiwa mikopo kwenye taasisi za fedha, ufumbuzi wake sasa umepatikana.
 Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mtaalaam wa kutengeneza Mfumo wa Utunzaji wa kumbukumbu kwenye Kompyuta, Erick Muta, alisema anashukuru kwa kupata tunzo hiyo ya dola za Kimarekani 328,000, zilizotolewa na Mfuko wa Ubunifu (ICF).
 Alisema hivi sasa wajasiriamali hao wanaweza kutunza kumbumbu zao za mapato na matumizi kila siku baadala ya kutumia madaftari kwa ajili ya kujua alichoingiza na alichotumi. 
 Mutta alisema mfumo huo (Min Shop), utawasaidia wafanyabiashara kwa kuwajengea uwezo utakaowafanya wakidhi vigezo vya kibeki ambapo watawza kukubalika katika kupatiwa mikopo kutokana na utunzaji bora wa kumbukumbu zao.
“Hadi sasa wapo baadhi ya wajasiriamali ambao wametumia mfumo huu ambao umewasaidia katika kupata mikopo toka tasisi za fedha, vilevile tunatarajia kuwatembelea watu mbalimbali kwa ajili ya kuwapatia elimu kuhusu mfumo huu jinsi unavyoweza kuwakwamua kiuchumi”alisema.
 Mkurugenzi wa Mfuko wa Sekta ya Ukuzaji Uchumi (FSDT), Sosthenes Kewe, alisema mpango  huo wa kuwajengea uwezo wabunifu na wajasiriamali ni endelevu ambapo hiyo, ni mara ya pili kutoa zawadi.
Alisema anaamini kuwa utasaidia katika kutanua wigo wa kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana, ambao ndio kilio kinacholikabili taifa.
Mmoja wa wafanyabiashara  Zephania Mgonella, alisema, tangu alipoanza kutumia mfumo huo ameweza kupata mafanikio katika utunzaji wa kumbukumbu zake, hata anapotakiwa taarifa za kila siku na mwezi anazipata kirahisi ambako hapo awali ilikuwa ni shida
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top