Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CHADEMA HALI SI SHWARI ..... WAMVUA UANACHAMA DIWANI WAO


 
 Na Elizabeth Ntambala
Sumbawanga
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinadaiwa kumvua uanachama wake Diwani wa kata ya Izia katika Manispaa ya Sumbawanga, Field  Kasitu kwa tuhuma ya kukisaliti chama hicho. 

 Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa Kasitu amefukuzwa baada yakuonekana akitambulishwa bungeni mjini Dodoma  akiwa mmoja kati ya viongozi  waliotoka mkoani Rukwa na kumsindikiza Mbunge wa Sumbawanga Mjini Aeshi Hilary baada ya kurejeshewa ubunge wake na Mahakama ya Rufaa kufuatiwa kutenguliwana Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga mwaka mmoja uliopita.

Tukio hilo lilionekana kuwakera baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA ambao walihoji kuwa iweje Diwani huyu ajiunge na CCM katikakushangilia kushinda kesi na kurejeshewa nafasi yake Mbunge huyo ihali wao CHADEMA kupitia aliyekuwa mgombea wao Nobert  Yamsebo kupinga ushindi wake.   
                         
 Pamoja na tuhuma hizoKasitu alisema kuwa wanaomlaumu juu ya hilo ni wachanga wa kisiasa na hawajui  mtazamo wake katika maisha yake ya kisiasa.

Kauli hizo za Kasitu zilionekana kuzidi kuwakera viongozi wake wa wilaya ambapo walimwandikia barua ya kumtaka kujieleza kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kosa la kudaiwa kufanya usaliti.
  Hatua hiyo ilielezwa kushikiwa bango na Katibu wa chamahicho ngazi ya wilaya Omeli Nkulu ambaye alimwandikia barua.

Mmoja ya wajumbe wa Kamati Tendaji ya wilaya ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa licha ya kutakiwa kujieleza tayari Diwani huyo ameandikiwa barua ya kuvuliwa uanachama japokuwa wapo baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo ambao wanaopinga hatua hiyo. 

Katibu CHADEMA  mkoa Ozemu Chapita alipoulizwa juu ya sakata hilo alisema kuwa anafahamu kuwa Kasitu alipewa barua ya kujieleza ndani ya siku 14,lakini haungi mkono hatua ya kuvuliwa uanachama.

"Mimi binafsi siungi mkono hatua ya kumvua uanachama kwani itatufanya tugawanyike katika kipindi hiki, jambo nisingependa lilotekee kwetu."alisema Chapita.

Kasitu ni Diwani aliyepata nafasi hiyo akitokea CCM ambapo alijiunga na CHADEMA baada ya kile kinachodaiwa kufanyiwa mizengwe wakati wa mchakato wa kura za maoni na kukosa nafasi ya kugombea kupitia chama hicho, hivyo kuamua kujiunga na CHADEMA na kumbwaga mpinzani wake kutokea CCM Timoth Makaza.
Mwisho.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top