Kamanda wa Kikosi cha
Usalama Barabarani – DCP. Mohammed R. Mpinga akiongea na kuwaasa madereva wa
Bodaboda wakati wa kufunga mafunzo hayo. Kushoto kwa Kamanda ni Rais wa AAT Mr
Nizan Jivan, CEO wa AAT Mr Yusuf Aghor na Mweka hazina wa AAT Mr
Pepe.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP
Mohammed Mpinga akikabidhi
cheti kwa mhitimu Mwanamke aliyehitimu mafunzo ya
Elimu ya Usalama Barabarani yaliyotolewa kwa madereva wa Bodaboda Dsm na Kikosi
cha Usalama Barbarani kwa kushirikiana na AAT (Automobile
Association of Tanzania) kwa ufadhili wa chama cha mashindano ya Magari Duniani
(FIA) wakati ufugaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika Gongolamboto 10/07/2013.
Anayeangalia ni Rais wa AAT Mr Nizan Jivan
Mr Nizan Jivan Rais wa
Automobile Association of Tanzania (AAT) akiongea na madereva wa Bodaboda wakati
wa ufungaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika Gongolamboto – Dar es salaam
10/07/2013. Kulia ni Mr Yusuf Aghor CEO wa AAT na kushoto ni ASP Swai wa Makao
Makuu ya Traffic Dsm.
Mr Nizan Jivan Rais wa
Automobile Association of Tanzania (AAT) akipokea zawadi maalum kutoka kwa
wahitimu wa Mafunzo ya dereva wa BODABODA mkoani Dar es Salaam kama shukrani
yao ya pekee kwa kudhamini mafunzo haya bure kwa madereva wa Bodaboda, ufugaji
wa mafunzo ya elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Bodaboda ulifanyika
Gongolamboto Dsm tarehe 10/07/2013.
Kamanda wa Kikosi cha
Usalama Barabarani – DCP Mohammed R. Mpinga (kushoto) akikabidhiwa Tuzo maalum
ya ushiriki wake katika kusimamia mafunzo ya Bodaboda mkoa wa Dar es Salaam.
Tuzo hiyo alikabidhiwa na Rais wa Automobile Association of Tanzania (AAT) Mr
Nizani Jivan wakati wa ufungaji wa mafunzo ya elimu ya Usalama Barabarani kwa
madereva wa Bodaboda tarehe 10/07/2013 Gongolamboto – Dar es
salaam.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani – DCP
Mohammed Mpinga akiwa katika
picha ya pamoja na Rais wa Automobile Association of Tanzania (AAT) na
wadau mbalimbali waliohudhuria katika ufugaji wa mafunzo ya elimu ya Usalama
Barabarani kwa madereva wa Bodaboda, tarehe 10/07/2013 Gongolamboto
- Dsm.
Kamanda wa Kikosi cha
Usalama Barabarani – DCP Mohammed R. Mpinga akikabidhi cheti kwa mmoja wa
wahitimu wa mafunzo ya Elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Bodaboda
katika ufugaji wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 10/07/2013 Gongolamboto –
Dsm.
Madereva Bodaboda wa mkoa
wa Dar es Salaam wakipokea kiapo chao cha utii kuashiria kuwa mafunzo ya Elimu
ya Usalama Barabarani waliyoyapata darasani sasa watayafanya kwa vitendo wawapo
katika kazi zao za usafirishaji wa abiria katika maeneo mbalimbali ya jiji la
Dar es Salaam. Kiapo hiki kilifanyika mbele ya Kamanda wa kikosi cha Usalama
Barabarani DCP Mpinga wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo kwa madereva wa
Bodaboda Gongolamboto 10/07/2013.
Sehemu ya Madereva Bodaboda
wa mkoa wa Dar es Salaam wakimsikiliza Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani
pichani hayupo wakati wa ufungaji wa mafunzo ya Elimu ya Usalama Barabarani kwa
madereva wa Bodaboda. Ufugaji wa mafunzo hayo ulifanyika Gongolamboto tarehe
10/07/2013.
Imechotwa: michuzi matukio
Post a Comment