Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SIMBA DAY YASOGEZWA MBELE

Na Mahmoud Zubeiry, wa Bin Zubeiry
 
TAMASHA la kuazimisha siku ya Simba SC linaweza kusogezwa mbele kwa simu mbili, kupisha sikukuu ya Eid El Fitri hivyo kufanyika Agosti 10, badala ya Agosti 8, kama ilivyo kawaida yake.
Aidha, mpango wa Simba SC kucheza na mabingwa wa Afrika mara nne, Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umeshindikana kutokana na timu hiyo ya Lubumbashi kutingwa na michuano ya Kombe la Shirikisho.
Simba SC

Na kwa sababu hiyo, timu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo, Dar es Salaam sasa itacheza na SC Villa ya Uganda katika tamasha hilo, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba ilitumai kucheza na Mazembe yenye wachezaji wake wa zamani wawili, Mbwana Samatta na Patrick Ochan ambao iliwauzua klabu hiyo miaka miwili iliyopita, lakini ratiba ya michuano ya CAF imeharibu mambo. 
Katika maendeleo mengine, wachezaji wa Simba SC waliokuwa na kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wanatarajiwa kujiunga na wenzao kambini, Bamba Beach, Kigamboni kuanzia leo jioni.
Wachezaji waliokuwa Stars ni viungo Amri Kiemba na Haroun Chanongo. Kiemba alicheza dakika zote 90 na kufunga la Stars ikilala 3-1 Uwanja wa Mandela, Namboole na kutolewa jumla ya mabao 4-1, baada ya awali kufungwa 1-0 Dar es Salaam wiki mbili zilizopita, wakati Chanongo aliingia uwanjani dakika ya 78 kumpokea John Bocco ‘Adebayor’ wa Azam FC.    
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top