Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Hivi ndivyo Gari la kubebea wagonjwa lilivyokamatwa likitumika katika wizi ndani ya Mgodi wa Geita

 

Mwandishi wa habari Denice Stephano anaripoti kwamba gari la kubebea wagonjwa limekamatwa likitumika katika wizi ndani ya mgodi wa Geita na kufanya wapatikane watuhumiwa tisa wa kesi ya wizi wa mafuta katika mgodi huo wa Dhahabu ( GEITA GOLD MINE ).

Mwendesha mashitaka wa polisi Inspekta Abiner ameiambia mahakama September 9 2013 kwamba 5/09/2013 saa 7:30 usiku huko eneo la Geita power ndani ya mgodi wa Geita gold mine watuhumiwa waliiba mafuta lita 630 ya dizeli, kula njama za kuiba mafuta hayo na kuharibu mali ambayo ni gari la kubeba wagojwa katika kituo cha Afya cha Nzera kwa kuling’oa viti...

Mtuhumiwa wa kwanza Hamudi Biemo (28) Dereva wa gari anatuhumiwa makosa matatu likiwemo la kula njama na kung’oa viti vya gari.
1
Abiner ameongeza kuwa washitakiwa hao walitumia gari aina ya Land Crusser yenye namba za usajili T 671 AKW mali ya Halmashauri ya wilaya ya Geita na kuingia mgodini kuiba mafuta aina ya Diesel lita 630 yenye thamani ya Tsh. 1,386,000/= mali ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM)


Waliofikishwa mahakamani ni Hamudi Biembo dereva wa gari la wagonjwa ,Malemo Paul (31) mkazi wa mtaa wa Mseto Geita,Selemani Magoso (31 )ambaye ni dereva pikipiki mkazi wa mtaa wa Shilabela Geita, Julias Boazi (28) mkazi wa Msalala road Geita ). Wengine ni Rashid Hussen (27) -Mlinzi wa mgodi, Ismail Zuber (26) -mlinzi wa Kampuni ya G4S ,Christoper Kombo -Operator wa GGM,Joseph Chiristopher (27) -Operator wa GGM
2
Wakili wa upande wa utetezi Leonard Bitemo baada ya watuhumiwa kusomewa mashitaka yao na kukana, aliiomba Mahakama ya wilaya kuahirisha kesi hadi wiki tatu ili wateja wake ambao ni Selemani Magoso, Boaz Paul na Milemo Paul wapate nafasi ya kujiandaa kwa ajili ya utetezi....


Madai hayo yalipingwa na mwendesha mashtaka wa poisi na kuomba mahakama ipange siku za karibu badala ya wiki tatu kwani kuna mashahidi ambao wanasafiri kwenda nje ya nchi, kesi hiyo itajwe 12/09/2013 ambako watakuwa wamejiandaa na mahakama ilikubaliana na uamuzi huo na washitakiwa wote (9) wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti.
3
4
5
6
7
8
10
11
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top