
Nape alisema kitendo cha mbunge huyo kuungana na
vyama vingine kupinga suala hilo ni kumdhalilisha Rais Jakaya Kikwete
aliyemteua kuwa mbunge kwa kumwamini kuwa mchapakazi, huku akiongeza
kuwa kitendo hicho ni unafiki mkubwa.
Nape aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara
wilayani Bariadi Mkoa wa Simiyu katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM
Taifa, Abdulrahman Kinana kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM.
Alisema Mbatia aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa
mbunge kutokana na kuonekana kuwa mchapakazi, huku akiongeza kuwa
kitendo alichokionyesha mbunge huyo ni kumgeuka Rais kama kinyonga
Nape alienda mbali zaidi na kuongeza kuwa hatua ya
mbunge huyo kuungana na wapinzani siyo sahihi na haikubaliki hata
kidogo, huku akimtaka kujiuzulu nafasi aliyopewa kwa heshima na Rais,.
Katibu huyo mwenezi aliongeza kuwa viongozi wa
Chadema wakiwemo Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, Dk Willbrod Slaa pamoja
na Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,Tundu Lisu, wamekuwa
wakitumia matatizo ya Watanzania kama mtaji wao wa kisiasa na kwamba
viongozi hao hawana aibu.
MWANANCHI
MWANANCHI
Post a Comment