Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UONGOZI WA HOSPITALI YA ZAKHEIMU WATOA UFAFANUZI WA TUHUMA YA MJAMZITO

 

    
Makiungu-hospital-TanzaniaNA MAGRETH    KINABO- MAELEZO
UONGOZI wa  hospitali  ya Mbagala  Rangitatu (Zakhem) iliyopo jijini Dar es Salaam umesema  kwamba  si kweli mama mjamzito alifukuzwa  usiku wa manane kama ilivyoripotiwa na gazeti  moja la kila siku la hapa nchini  hivi karibuni.
 
Kauli  hiyo ilitolewa leo na Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo,Dk. Julius Nyakazilibe katika taarifa yake kwa vyombo baada ya uchunguzi wa tukio hilo kufanyika,ambao umehusisha mama mjamzito huyo  wakiwemo ndugu wa mlalamikaji ikiwemo nesi wa  na daktari wa zamu.
 
 Ambapo alisema Mei 31, mwaka huu mama huyo mjamzito  ,Ashura  Omary  alifika hospitalini  hapo  majira ya saa sita usiku akiwa na ndugu zake  walimkuta nesi wa zamu kwenye wodi ya wakina mama, lakini kabla ya kupokelewa aliingia mama mwingine mjamzito mwenye kifafa cha  mimba.
 
“ Kutokana na sababu za kiutaalamu nesi wa zamu alianza kumuhudumia mama mwenye kifafa cha mimba, hali hiyo ilimfanya Ashura kuanza kulalamika  kuwa hakuhudumiwa wakati yeye alikuwa wa kwanza kuingia. Kitendo hicho kilimfanya nesi huyo amweelekeze wodini kupumzika na kusubiri.
 
Dk. Nyakazilibe alifafanua kuwa Ashura alipofika wodini alikuta vitanda vyote vimejaa na kukosa mahali pa kulala ambapo  aliendelea kusimama akimsubiri nesi,baada ya muda nesi huyo alienda  kumpima na kumwambia njia yake haijafunguka na uchungu haujaanza,hivyo alimwambia aende nyumbani na kurudi siku inayofuata  yaani saa tano asubuhi .
 
 Alisema baada ya kuambiwa hivyo Ashura alitoka nje na kumwambia mama yake aliyekuwa amemsindikiza kilichotokea ndani huku akimlaumu kuwa kwa nini walimleta  hopitalini hapo wakati tangu awali alitaka kwenda kujifungua  kwenye kituo cha Mbagala Kizuiani (Round  table). 
 
Baada ya majadiliano kati ya mgonjwa na ndugu waliomleta walikubaliana kuondoka na kwenda Mbagala Kizuiani usiku huohuo. Hivyo nesi wa zamu alipomaliza kumuhudumia mama mwenye kifafa aliingia wodini  ili amuhudumie lakini alimkuta hayupo alipouliza wagonjwa wengine  walisema ametoka nje kuongea na ndugu zake .
 
 Alisema nesi huyo  aliamua kumtafuta nje lakini hakumkuta mama huyo  wala ndugu zake.
 
Aidha Dk. Nyakazilibe alisema kutokana na maelezo hayo mama huyo aliondoka mwenyewe kitendo kilichotafsiriwa kuwa  hakutendewa haki na kusema kuwa amefukuzwa.
 
Kuhusu tuhuma ya mtoto mchanga kunyeshwa dripu ya maji Agosti 15, mwaka huu, alisema si za kweli kwani  mtoto  huyo hakuwa mchanga bali ana umri wa miaka miwili.
 
“ Si   kweli kuwa mtoto alinyeshwa maji ya dripu bali alipewa matibabu ya ORS(Oral Rehydration Salt). Mama aliagizwa kununua maji safi ili yaje kuchanganywa na dawa iliyotumika kumnyeshwa mtoto huyo baada ya kuona mgonjwa na uwezo wa kunywa maji wakati wauguzi wakiendelea kutafuta mishipa.
 
Aliongeza kuwa utaratibu huo ulifanyika kwa sababu za kiutaalam.
 
Uongozi wa hospitali hiyo umewataka wananchi yanapotokea malalamiko yoyote hospitalini hapo kutoa taarifa mara moja na si kusubiri muda upite. Pia umewataka waandishi wa habari  kupata maelezo ya kina wanapoandika habari.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top