Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI MULUGO AWACHARUKIA WASIMAMIZI WA MITIHANI

148_Philipo-Mulugo1NA ELEUTERI MANGI -MAELEZO

SERIKALI imewataka wasimamizi  watakaosimamia mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi  kufanya kazi yao ya kusimamia kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu, huku ikiwaonya wale  watakaokiuka  agizo hilo kuwa  watachukulia hatua za kisheria.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Philipo Mulugo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu mtihani huo, ambao unaotarajiwa kufanyika Septemba 11 na 12 mwaka huu.

“Napenda kuwaasa tena wasimamizi kujiepusha na vitendo hivyo vya udanganyifu kwani Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote atakayebainika kukiuka taratibu za mitihani” alisema Mulugo.

Naibu Waziri huyo alisema kuwa wapo baadhi ya wasimamizi ambao wamekuwa nawakishriki katika kuwasadia watahiniwa kufanya udanganyifu kwenye mitihani yao.

Katika mtihani huo jumla ya watahiniwa 868,030 wamesajiliwa kufanya mtihani huo, kati yao wavulana 412,105 sawa na asilimia 47.47 na wasichana 455,925 sawa na asilimia 52.52.

Naibu Waziri huyo aliendelea kusema kuwa  kuna jumla ya watahiniwa 844,810 ambao wanatarajiwa kufanya mtihani huo kwa lugha ya Kiswahili kati yao wavulana 400,335na wasichana 444,475. Wanafunzi 22,535 kati yao wavulana ni 11,430 na wasichana ni 11,105 watafanya mthani huo kwa lugha ya Kiingereza ambao ndio waliyokuwa wakiitumia kujifunzia.

Kwa upande wa watahiniwa wasioona, waliosajiliwa kufanya mtihani huo ni 88 wakiwemo wavulana 56 na wasichana 32. Watahiniwa wenye uoni hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa ni 597. Wanaotarajiwa kufanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili ni watahiniwa 546 kati yao wavulana ni 263 na wasichana ni 283. Wanaotarajiwa kufanya mtihani kwa lugha ya Kiingereza ni watahiniwa 51 kati yao wavulana ni 21 na wasichana 30.

Aidha, Mulugo alisema kuwa maandalizi yote kwa ajili nya mtihani huo yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mtihani, kusambazwa kwa fomu maalum (Optical Mark Reader, (OMR) za kujibia mtihani na nyaraka zote muhimu zinazohusika.

Akijibu swali lililoulizwa na waandishi wa habari katika mkutano huo juu ya watahiniwa kutumia fomu za OMR kujibia mtihani Naibu Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani Tanzania Dkt. Charles Msonde alisema kuwa wanafunzi wameandaliwa vizuri kutumia fomu hizo na zimeonesha mafanikio makubwa.

Dkt. Msonde alisema katika kipindi cha  mwaka 2012 fomu zote zilizotumika kujibia mtihani huo zilipita vizuri kwenye kompyuta na ambazo ziligoma kutokana na sababu mbalimbali zilisafishwa na kunyooshwa na hatimaye kukamilika na kusahihishwa.

Masomo yatakayotahiniwa katika mtihani huo ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi ,Hisabati na maarifa ya jamii.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top