Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BAKWATA LAMALIZA MGOGORO WILAYA YA ARUMERU

               

8011905_orig_16154.jpg
Kushoto ni Mjumbe wa baraza la mashehe wilaya ya Arumeru, Haruna Hussein Lotta, pembeni ni viongozi wa zamani wakikabidhiana rasmi ofisi (picha: JamiiBlog)
*******
BARAZA kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limetatua mgogoro uliokuwepo kati yao na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Arumeru na Katibu wa Wilaya wa baraza hilo baada ya kusimamishwa nafasi zao za uongozi kwa miezi saba.
Kaimu katibu wa (BAKWATA) mkoa wa Arusha, Abdallah Masoud alisema kuwa bazara hilo limefikia hatua ya kuwarudisha.
       
viongozi hao kwenye nafasi zao baada ya kusimamishwa katika nafasi hizo kutokana na ukwiukaji wa sheria walioufanya wakiwa madarakani kinyume cha sheria cha baraza hilo.
Alisema kuwa, baada ya baraza kuu kukaa na kufanya vikao vyake, walipitia barua mbalimbali zilizoandikwa na viongozi hao za kuomba kurudi katika nafasi hizo huku wakikiri kutorudia tena makosa waliyofanya ndipo baraza hilo lilipopitia na kuwarudisha tena katika nafasi.

'Sisi dini yetu inaturuhusu kusamehe na kuwasikiliza watu mbalimbali katika shida zao ikiwemo kutatua migogoro mbalimbali iliyopo katika misikiti yetu lengo likiwa ni kuhakikisha kila mmoja wetu anaishi kwa amani na kuondoa tofauti miongoni mwa waumini wetu kwani ndio lengo letu la kuleta amani kwa waumini na viongozi wetu kwa ujumla' alisema Kaimu katibu huyo.
Masoud aliwataka viongozi hao pamoja na mashehe mbalimbali kuhakikisha wanahubiri amani katika maeneo yao sambamba na kuondoa migogoro iliyopo miongoni mwao na hatimaye kuweza kuishi kwa amani na upendo ili kufikia malengo waliyojiwekea.
Naye Mjumbe wa baraza la mashehe wilaya ya Arumeru, Haruna Hussein Lotta alisema kuwa, aliwataka viongozi mbalimbali wa dini hiyo kuacha majungu na unafiki badala kwani kwa kufanya hivyo ndio wanazidi kuliharibu baraza hilo badala ya kulijenga.
Haruna alisema kuwa,waislamu wengi sasa hivi wameishia kukaa na kupiga majungu na kusengenyana hali ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa sana kuleta mpasuko ndani ya baraza la bakwata wilaya ya Arumeru.
Aliongeza kuwa, endapo viongozi wa dini hiyo pamoja na waumini hawataepuka masengenyo na majungu katika baraza hilo wataendelea kuwa na migogoro ambayo haitaisha, hivyo kuwataka kukaa na kuacha tofauti zao kwa muda huu ambao viongozi wamerudishwa katika nafasi zao na hivyo kulijenga baraza hilo ili lidumu na kuwa na amani toafuti na ilivyokuwa hapo awali.
Aidha waliorudishwa katika nafasi zao ni Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Arumeru ,Jumanne Zuberi na katibu wa wilaya Ramadhani Kumallah ambapo aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo ya Mwenyekiti ni Yahaya Hajji na Katibu alikuwa Yahaya Mwengellah.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top