Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

LOWASSA ACHANGISHA ZAIDI YA MILIONI 233 ZA MADAWATI KWA SHULE ZA SEKONDARI

 Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa akiwasili katika viwanja vya Shule ya Mtakatifu Antony's Mbagala tayari kuendesha harambee ya kuchangia madawati kwa shule za Tarafa ya Mbagala ambapo jumla ya Tsh. Milioni 222 zilipatikana. Picha na Emmanuel Shilatu
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa akifungua zoezi la uchangiaji wa harambee ya kupatikana kwa madawati ya Tarafa ya Mbagala ambapo aliisihi sana jamii kujitoa ili kukamilisha mahitaji muhimu ambayo ni changamoto kwa shule za kata pasipo kuisubiria mpaka serikali kufanya.

 
 Mbunge wa Kigamboni, Mhe. Faustine Ndugulile akiisihi sana jamii haswa Wazazi kujenga mazoea ya kufuatilia kwa ukaribu elimu za Watoto wao mara kwa mara.
 
Mbunge wa Temeke, Mhe. Abbass Mtemvu akitoa ahadi yake ili kufanikisha upatikanaji wa madawati mashuleni huku akisikilizwa kwa umakini mkubwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Lowassa.
 Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Hassan Zungu alichangia milioni 5 katika harambee hiyo. Picha na Emmanuel Shilatu.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa akipokea michango mbalimbali ya wazazi wenye uchungu dhidi ya watoto wao wanaoketi chini mashuleni. Picha na Emmanuel Shilatu

 Wanafunzi nao hawakuwa nyuma kuchangia upatikanaji wa madawati ambapo jumla ya pesa Tsh. Milioni 222 zilipatikana.





Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa akiwa vyeti mbalimbali kwa wahitimu kidato cha nne wa shule 12 wa sekondari za Tarafa ya Mbagala.

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa alikabidhiwa zawadi na kamati ya maandalizi ambapo zawadi hiyo ilikabidhiwa na Mwenyekiti wa kamati

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Ngoyai Lowassa akiwa kwenye picha ya pamoja na Waalimu wakuu wa shule za sekondari za Tarafa ya Mbagala, viongozi waliokuwepo pamoja na Wajumbe wa kamati ya maandalizi. Picha na Emmanuel Shilatu
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top