Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UWT YAWAHAMASISHA WANAWAKE

 


SONY DSC
Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kindondoni, Bi. Florence Masunga akihutubia kwenye mkutano wa UWT ulifanyika Octoba 19-2013 kwenye Kituo cha Mabasi ya Daladala cha Mwenge jijini Dar se Salaam lengo ni kuwahamasisha wanawake nchini kudumisha upendo na amani na kujiletea maendeleo. SONY DSC
Katibu wa wa UWT Wilaya ya Kindondoni, Bi. Huba Issa akihutubia katika mkatano huo SONY DSCMwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge akitoa neno kwa wanachama wa CCM na wananchi waliohudhuria kwenye mkutano huo.
SONY DSC
Msanii wa Kundi la Taarab la Five Star, Siwai akiimba kwenye mkutano huo. SONY DSCWanachama na viongozi wa CCM wakiwa kwenye picha ya pamoja, (mwenye pensi nyeupe) ni Mwenyekiti wa CCM Tawi la Mwenge, Bw. Kessy Tuyuyu. SONY DSCWanachama wa UWT na wananchi wa kawaida wakiwa kwenye mkutano huo. SONY DSC  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida,akiwaonyesha wanachama wa CCM kadi ya CHADEMA mara baada ya kukabidhiwa.SONY DSCWanachama wapya wakila kiapo,(wa pili kushoto) Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida akiwaongoza wanachama katika zoezi hilo.
Picha, Habari na Philemon Solomon wa fullshangwe Dar es Salaam
     Umoja wa Wanawake (UWT) Kata ya Kijitonyama, jijini Dar es Salaam umetoa rai kwa wanawake kote nchini  kujitokeza kwa wingi kwenye chaguzi mbalimbali ili Chama cha Mapinduzi kiendelee kuongoza nchi.
Rai hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa umoja huo Wilaya ya Kinondoni, Bi. Florence Masunga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kituo cha Mabasi ya Daladala cha Mwenge jijini Dar se Salaam uliokuwa na lengo la kuwahamasisha wanawake nchini kudumisha upendo na amani na kujiletea maendeleo.
Masunga alitoa kauli hiyo wakati akijiandaa kumkaribisha mgeni rasmi wa mkutano huo, Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida ambapo alisema wanawake ndiyo wanaoweza kuifanya CCM kuendelea kuongoza.
“Nawaomba wanawake mjitokeze kwa wingi katika uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu kuliko ilivyokuwa huko nyuma,” alisema Masunga.
Naye Katibu wa UWT Wilaya ya Kinondoni, Huba Issa alikisifia Chama Cha Mapinduzi kwamba ndicho pekee kinachopaswa kuongoza nchi na siyo vyama vya upinzani.
Katibu huyo aliongeza kwamba kama Watanzania wanataka kuendelea kuishi kwa  amani hawana budi kuachana na wapinzani ambao hawana sera nzuri kama za CCM.
Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Bw. Salumu Madenge akizungumza kwenye mkutano huo alisisiza Watanzania kuzidi kukichagua Chama Cha Mapinduzi kwa sababu kina sera nzuri na ndicho kilicholeta maendeleo yanayoonekana.
“CCM imejenga shule, barabara, hospitali ambapo hivi sasa tunasafiri kutoka Feri hadi Mwanza kwa kupita kwenye lami zinazoteleza…inashangaza sana unapomuona mtu anaibuka na kusema CCM haijafanya kitu chochote,” alisema Madenge.
Baada ya kumkaribishara mgeni rasmi, Madabida, naye kama wenzake waliomtangulia alisisitiza wananchi kuendelea kukichagua Chama cha Mapinduzi ili kiendelee kuongoza nchi.
“Jamani kila mtu anayaona mambo yaliyofanywa na CCM kuanzia awamu ya kwanza ya Mwalimu Nyerere ambaye alijenga umoja na mshikamano wa kitaifa na msingi wa amani, awamu ya pili ya Rais Mwinyi alitoa ukilitimba na kuleta mfumo wa uchumi uria,” alisema Madabida na kuongeza:
“Awamu ya tatu ya Rais Mkapa alileta uchumi wa kisasa wa kujitegemea na awamu ya nne imeleta kasi ya maendeleo ya watu na nchi kwa ujumla.”
Katika mkutano huo, kijana Rashid Shabaan aliyekuwa mwanachama wa Chadema, aliachana na chama hicho na kujiunga na CCM, pia wanawake kadhaa walikabidhiwa kadi za CCM baada ya kujiunga na chama hicho ambapo walikula kiapo cha utii.
Kabla ya kufanyika kwa mkutano huo, lilifunguliwa tawi la UWT la Ally Maua. Mkutano huo ulihudhuriwa pia na baadhi ya wanachama wa CCM kutoka Zanzibar na ulipambwa na burudani za muziki.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top