Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

AUAWA KIKATILI KWA KUPIGWA MAPANGA





MKAZI wa Kijiji cha Kapalala Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi , Mele Seni (60) ameuawa kikatili kwa kukatwa mapanga kichwani na mgongoni na watu wasiofahamika wakati akiwa nyumbani kwake akiota moto, sababu kubwa ikielezwa kuwa mzee huyo alikuwa anatuhumiwa kwa ushirikina.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea jana saa moja na nusu usiku wakati Seni akiwa anaota moto nyumbani kijijini hapo.

Alisema siku hiyo ya tukio Seni akiwa nyumbani kwake amejipumzisha akiota moto ghafla walitokea watu wasiofahamika na kupiga hodi nyumbani kwa Seni ambapo aliwakaribisha akidhani ni watu wema.

Inadaiwa ndipo watu hao wakiwa na mapanga walipoanza kumshambulia Seni kwa kumkata kwa panga kwenye kichwa na mgongoni huku akipiga mayowe kuomba msaada kwa majirani zake.


HABARI LEO
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top