Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

PSPF yaanza kukopesha nyumba wanachama wake

 

Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Bw. Chaha Nyaikabwe  akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mpango wa Mfuko huo kuanza kukopesha nyumba kwa wanachama wake kwa ajili ya kuboresha huduma zake na kutatua changamoto za makazi kwa wanachama,wakati  wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari( MAELEZO) leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Mawasiliano, Masoko na Uenezi Bi. Hawa Kikeke.
 
*****
(Picha na Hassan Silayo)
 
Na Frank Mvungi-Maelezo
Mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma (PSPF) waanza kukopesha nyumba wanachama wake ikiwa ni moja ya hatua za kuboresha huduma zake kwa wanachama.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Kaimu Mkurugenzi wa uendeshaji na Meneja kumbukumbu wa mfuko wa Resheni kwa watumishi wa umma  Bw. Chacha Nyaikwabe wakati wa mkutano na waandishi wa habari .
Akifafanua zaidi alisema mfuko huo umejenga nyumba katika mikoa ya Shinyanga nyumba 50,Mtwara nyumba 50 na Morogoro nyumba 25 ambapo lengo la Mfuko huo ni kufika mikoa yoye hapa nchini.
Aliongeza kuwa nyumba hizo zinakopeshwa kwa wanachama wa mfuko huo ambao wanatakiwa kulipa mkopo wa Nyumba hizo kwa muda wa miezi 300.
Alibainisha kuwa hata wananchi wasio wanachama wanaweza kununua nyumba hizo ambazo kila moja inagharimu  kuanzia milioni 59 hadi milioni 80 kutegemeana na ukubwa wa nyumba.
Alitoa  rai kwa wananchi wote kujiunga na mfuko huo bila kujali wako katika sekta rasmi au isiyo rasmi ili waweze kunufaika na mafao mbalimbali yanayotolewa na mfuko huo ikiwemo fao la elimu,Kifo, kujitoa na Ugonjwa.
Aliongeza kuwa katika kuboresha huduma zake mfuko huo sasa umeanza kusajili wanachama katika mpango wa hiari kwa raia na asiye raia wa Tanzania ambapo mwanachama anaweza kuwasilisha michango yake kwa wiki, mwezi au msimu.
Katika hatua nyingine Mfuko huo umeanzisha utaratibu unaowawezesha hata wasio wananchi walio nje ya Tanzania kujiunga na mfuko huo ilimradi tu wawe watanzania.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top