Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Finland yapongeza `Matokeo Makubwa Sasa`

 
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimuongoza Waziri Mkuu wa Finland, Jyrki Katainen (katikati) alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam jana ili kujionea shughuli mbalimbali za bandari hiyo kubwa kabisa Afrika Mashariki.
**********
Waziri Mkuu wa Finland, Jyrki Katainen, amesema Mpango wa Maendeleo Makubwa Sasa uliobuniwa na Rais Jakaya Kikwete, unaifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa ya kisasa zaidi na kwamba  sekta binafsi zina umuhimu mkubwa katika suala hilo.

Waziri Katainen alisema hayo wakati wa ziara yake aliyoifanya jana katika Bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya kuangalia ufanisi wake na kuendeleza uwekezaji wa Finland nchini.

Katika ziara hiyo, kiongozi huyo wa Finland aliambatana na maafisa wa serikali ya nchi yake, Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Filberto Sebregondi, Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo na  Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Charles Palangyo.

“Mkakati wa Rais wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now), huongeza kasi ya mchakato wa kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa ya kisasa zaidi. Wajibu wa sekta binafsi katika kufanikisha hili ni wa muhimu sana. Pia ninayo furaha kuona uwekezaji wa Finland kupitia kampuni zinazofanya kazi bandarini hapa,” alisema kiongozi huyo wa Finland.



Waziri Mkuu  Katainen, pia aliipongeza jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali ya Tanzania katika kuboresha miundombinu ya bandari na usimamizi mzuri wa kuongeza ufanisi wa utoaji huduma bandarini hapo.

Kwa upande wake, Balozi Sebregondi, alisema, Umoja wa Ulaya  umenuia kuwa mshiriki hai wa mazungumzo yanayohusu maendeleo ya biashara na sekta binafsi, ikiwa ni pamoja na mchakato huo wa kuifanya bandari hiyo kuwa ya kisasa zaidi,  kati ya Mamlaka ya Bandari ya nchini (TPA) na umoja huo.

Ziara ya kiongozi huyo nchini ambayo ilimalizika jana, ililenga kudumisha uhusiano baina ya Tanzania na Finland na kuhamasisha  maendeleo ya kibishara kati ya kampuni za kibiashara za mataifa hayo.
 

CHANZO: NIPASHE
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top