Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KATIBU MPYA WA CCM IRINGA MJINI ATUA KWA KISHINDO ASEMA MBUNGE MSIGWA MWISHO WAKE UMEFIKA


Aliyekuwa mbunge Iringa mjini Monica Mbega kushoto na  kulia mbunge Msigwa baada ya  kumpokea ubunge Mbega

Katibu mpya  wa CCM Iringa mjini Hassan Mtenga



Wafuasi  wa Chadema  wakirudisha kadi  kwa katibu wa CCM Iringa mjini jana


Katibu  wa CCM Iringa mjini Hassan Mtenga akimhoji mmoja kati ya wana Chadema aliyerudisha kadi na kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara  jana 






Mbunge Ritta kabati kulia akimsaidia mmoja kati ya makada wa Chadema kuonyesha kadi  baada ya kujitoa Chadema na kujiunga na CCM jana  kushoto ni mwenyekiti wa CCM wilaya Abed Kiponza

Viongozi wa CCM  wakipiga picha ya pamoja na wana chadema  waliojiunga CCM






Mwenyekiti wa CCM Iringa mjini Abed Kiponza kulia akipokea kadi kwa  wana Chadema  waliojiunga CCM jana











CHAMA Cha mapinduzi (CCM) wilaya ya  Iringa mjini  kimesema kimejipanga kwa nguvu zote kuhakikisha mbunge wa  jimbo hilo mchungaji Peter Msigwa anaachia jimbo hilo hata kama hataki ikiwa ni  pamoja na  wiki tatu kwa mstahiki meya  wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa Amani Mwamwindi kufuatilia kero mbali mbali za wananchi ikiwa ni pamoja na kujua kiasi cha Tsh milioni 15  zinazotolewa kwa  ajili ya mfuko wa  maendeleo ya  jimbo hilo kama zinatumika vema .

Mbali ya  hilo pia  kufuatilia huduma  zinazotolewa katika vituo  vya afya  Hospital na Zahanati kama zinafanyika kwa ubora  ama  zinafanyika kwa kuwanyanyasa  wananchi.

"Ushindi  wa  Msigwa  jimbo la Iringa mjini ulitokana na CCM wenyewe ila  sasa tunasema kamwe hatutarudia makosa yaliyojitokeza ni lazima turudishe  jimbo na Msigwa fedha zake azitumie  vema asijaribu kuingia katika ubunge tena"

  katibu wa CCM Iringa mjini Hassan Mtenga  aliyasema  hayo  juzi wakati wa mkutano wake wa kwanza uliofanyika katika  uwanja wa Mwembetogwa toka alipohamishiwa wilaya ya Iringa mjini akitokea Hai mkoani Kilimanjaro
 Alisema zama za ubunge wa Mchungaji  Msigwa katika jimbo la Iringa mjini umekwisha na sasa atake ataondoka na asipotaka ataondoka. 
"Mwambieni mbunge Msigwa wakati  wa kuwadanganya  wananchi umekwisha  na lazima sasa awaeleze  wananchi  wa jimbo la Iringa mjini  wapi  anapelekea  fedha za mfuko wa  jimbo ambazo  zinatolewa kila mwezi na Rais Jakaya  Kikwete"
Hata  hivyo alimuagiza meya  kupambana ili  fedha  kiasi cha Tsh milioni 15  zinazotolewa na rais Kikwete kuona zinafanya kazi gani katika ofisi ya mbunge  pia kutembelea  Hospital  na vituo vya afya  ili  kuona changamoto mbali mbali ndani ya wiki tatu kupeleka majibu katika ofisi yake.

 
Kuhusu  kupanda kwa gharama za umeme ni matokeo ya Dr Slaa ambae  alipigia kelele suala la Richmond na  Dowans ambapo baadhi ya  wabunge  waliunga mkono  suala  hilo ila leo baada ya mambo kuwa magumu tunalalamikia suala  hilo ambalo waasisi  wake ni Chadema kuleta kwele .

Alisema  kuwa  tunahitaji  vijana  kuleta maendeleo  ya mji wa Iringa na sio vijana  wa kutumiwa kuvuruga maendeleo ya mji wa Iringa.
" Nawaombeni  wananchi  kuwa tayari  tumemshika pua mbunge Msigwa na naomba  wananchi tusaidiane  kumnywesha panado na ninamuomba  Msigwa fedha za kiinua mgogo  zake asije  tena katika jimbo la Iringa mjini atumie  kwa kazi nyingine  ....tumeanza mkakati  huu kwa ajili ya kumnyoa Msigwa "

Katika  mkutano  huo  wananchi   walipewa nafasi ya  kuwaweka  kitimoto madiwani  wao ili kujibu kero  mbali  mbali za  katani kwani  huku  wananchi  wa  jimbo  hilo la Iringa  mjini  wakikitaka  chama hicho kusaidia  kukinusuru  chama  na  kura  za chuki  kutokana na shirika la ugavi  wa umeme nchini (TANESCO)  kuendelea  kupandisha  gharama  za  umeme.

Wananchi  hao  walisema  kuwa  ili CCM jimbo  hilo na Tanzania kwa ujumla kiweze  kushinda katika uchaguzi  mkuu wa mwaka 2015  na ule wa  serikali za mitaa utakaofanyika mapema mwaka  huu ni lazima gharama  za umeme ishuke


Kwani  walisema  kuwa  hatua ya  TANESCO  kuendelea  kuongeza  bei ya  umeme  ni  kuongeza  ugumu  wa maisha  kwa  watanzania na kuwa ushindi  wa CCM  utatokana na utetezi  wa chama katika  kuwaondolea  mzigo  wa bei ya umeme watanzania.

Mbali  ya  hilo pia  wananchi  wa  kata ya Kihesa walimbana  diwani  wao Bw  Mussa Wanguvu  kutokana na hatua ya  kushindwa  kupigania  wananchi ambao  wanatakiwa  kuvunja  nyumba  zao ambazo  zimejengwa katika eneo la  Semtema Majengo  mapya eneo ambalo halitakiwi  kisheria

Diwani  Wanguvu  akijibu  swali  hilo alisema  kuwa eneo  hilo  lilizuiwa baada ya kufanyika kwa mkutano wa hadhara  hasa  wale  ambao  wamejenga katika mlima na wapo hatarini  kuangukiwa na mawe  ila baadhi ya maeneo ambayo  si  rasmi  ni waliachiwa .

Kwa  upande  wao  wananchi  wa kata ya Mtwivila  walimtaka diwani  wao Bw  Victor Mushi  kueleza  ni  lini atatekeleza ahadi yake  ya zahanati na ubovu  wa barabara katika  eneo la Mkimbizi pamoja .

Kwa  upande  wake diwani Mushi  kuhusu  suala  la ujenzi  wa  kituo cha afya  alisema  kuwa ahadi hiyo haikuwa ya kwake  ila  ilikuwa katika ilani  ya  CCM  japo alisema ujenzi  wa  mradi huo  upo mbioni  baada ya  kumaliza miradi ya zamani utaanza mradi huo  wa ujenzi  wa  kituo cha afya.

Kuhusu  barabara  alisema  kuwa kata  hiyo  wamejitahidi  kutengeneza  mifereji na zaidi ya Tsh  bilioni 1.8  zitatengeneza  barabara  ya lami  kutoka Mtwivila  kwenda Mkwawa  na tayari  zoezi hilo linaendelea.

Katika  hatua  nyingine  Mushi  alipinga  madai ya  wananachi  kuwa  uongozi  wa Halmashauri  ya Manispaa ya  Iringa  umekuwa  ukifanya usafi  katika mji  kutokana na kuwepo kwa ugeni ama  vikao  kuwa jambo  hilo  si kweli na kuwa linafanyika kulingana na bajeti  na ufinyu  wake.


Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati pia aliweza kueleza  kazi mbali mbali alizozifanya katika jimbo la Iringa mjini ikiwa ni pamoja na kujenga kituo cha polisi kwa gharama zake eneo la Tumaini na kuwa ataendelea kuchonga sana juu ya kero za wananchi wa Iringa mjini.

Kabati alisema kuwa kamwe hatarudi nyuma katika utendaji na kuwa siku zote atawapigania wananchi wa jimbo la Iringa mjini na kuwa kuwa siku zote kwake atahakikisha anatenda zaidi. 

 Akielezea mambo ambayo amepata kutekeleza alisema ni pamoja na kusaidia sekta ya elimu vitabu na kompyuta pamoja na kusaidia vikundi vya vikoba katika jimbo hilo la Iringa mjini.
Mstahiki  meya  wa Manispaa ya  Iringa Aman Mwamwindi  akijibu kero mbali mbali akianza na Hospital ya  wilaya ya Iringa  mjini alisema kuwa  Hospital  hiyo  imeendelea  kutoa huduma .

Huku  ujenzi  wa barabara  za lami katika mji  huo kupitia pesa za benk ya Dunia  alisema barabara  itajengwa kuanzia  Samora ,Hospital ya Frelimo , Itamba na maeneo mengine ya mji .

Kuhusu  suala la usafi  alisema  kuwa moja kati ya sababu  zilizopelekea mji wa Iringa  kutoshika nafasi ya kwanza ni kutokana na hadhi ya makaburi na ndio  sababu makaburi ya makanyangio  kuanza  kuzungushiwa  uzio ili  siku moja  Manispaa ya  Iringa  iweze  kushika nafasi ya kwanza .

Alisema kuwa ni vema  suala la maendeleo  ya mji wa Iringa lisifanyike kwa itikadi  za  vyama na badala  yake  kufanyika  kutokana na mazingira yaliyopo .

Kuhusu  suala la Stendi ambalo limeendelea  kuleta lugha mbali mbali kutoka serikalini na viongozi  wa kisiasa alisema  kuwa hashangai na kauli  za  upotoshwaji juu ya ujenzi wa stendi hiyo ya kisasa ya mkoa itakayogharimu  zaidi ya Tsh bilioni 4  fedha  kutoka benki ya  dunia .

Alisema  kuwa mchakato  wa ujenzi  wa  stendi  hiyo umeshirikisha  wadau  wote  nyeti hadi  mshauri  wa mambo ya kimazingira  kimataifa  na tayari ameifanya kazi  hiyo na  kutoa maelekezo  yake ya kitaalam ambapo ameruhusu ujenzi huo.
Alisema inapojengwa  stendi hiyo  kutoka ukingo wa mto ni mita zaidi ya 700 wakati sheria ya ujenzi ya Rufiji na Iruwasa ni mita kati ya 50 na 60 hivyo stendi  hiyo ipo mbali zaidi  kuliko sheria.

Alisema  kuwa fedha  za ujenzi  wa stendi hiyo hata kama Halmashauri ingekusanya isingeweza kupata  fedha  hizo ambazo hata kama ingekusanya kwa miaka  zaidi ya 3 bila kupata .

Alisema  kuwa  wanaotumia maendeleo  kwa ajili ya kutafuta umaarufu katika  siasa ni kutowatendea haki  wananchi ambao  unawatumikia na kuwa suala la uongo halikubariki katika dini  zote .

Hata  hivyo  Mwamwindi  alisema jitihada mbali mbali  zinazofanywa na serikali ya  CCM  katika manispaa ya  Iringa ni kutaka  kuiwezesha  Halmashauri  hiyo kuja kuwa jiji kama   ilivyo Mbeya, Mwanza na Arusha .

Hivyo  alisema tayari  jitihada mbali mbali  za  kuwezesha mji wa Iringa kuwa jiji na tayari  wamepeleka mradi  wa maji Nduli mradi  ambao wakati wa kuwekeana  saini  mbunge  wa jimbo la Iringa mjini alipata  kushiriki .

"Tumepeleka  barabara  kutoka Tumaini  kwenda  Kigonzile KM 6   tumepeleka mabati kwa ajili ya choo mgongo pamoja na kuweka  vituo katika eneo la Kigonzile  ili kupeleka huduma  hiyo kwa  wananchi ... kwa  hiyo ndugu zangu mheshimiwa Mushi amezungumzia  barabara  ya kutoka Mkimbizi hadi bima  kiasi cha mabilioni ya  fedha  ambazo binafsi sijapata  kusaini fedha nyingi kiasi  hicho ....sasa  tumeanzisha mkakati wa kugawa  viwanja na kupasua  njia na ninasema kuwa ujenzi  wa stendi upo pale pale na suala  hili lipo kwa waziri mkuu ambaye  ndie mwenye  TAMISEMI"
Wakati  huo huo  katika mkutano  huo  CCM ilipokea  wanachama  zaidi ya  10 kutoka Chadema ambao  walidai  wameamua  kurudi CCM baada ya kuona Chadema  kuna  ubabaishaji mwingi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top