
Kocha
mpya wa Yanga aliyewasili nchini majuzi kwa ajili ya kuja kufanya
mazungumzo na uongozi wa timu hiyo, Huns Plujim, akiwa uwanja wa ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati alipokuwa akiwasili nchini.
Wakati
yimu ya Yanga ikiwa bado ziarani nchini Uturuki kwa ajili ya mazoezi ya
kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na mechi za
Kombe la Mataifa Afrika, anayetarajia kuwa kocha Mkuu wa timu hiyo
amewasili nchi kwa ajili ya kufanya mazungumzo na uongozi wa Klabu.
Taarifa
za awali zilizokuwa si rasmi zilikuwa zikisema kuwa Klabu hiyo
ilihitaji huduma ya aliyekuwa Kocha wa Taifa Stars Mbrazil, Marxio
Maximo, ambaye kwa sasa amelipotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa
tayari imeshindikana kocha huyo kuja kukinoa kikosi cha Yanga kutokana
na kutoelewana kwa upande wa malipo kwa dau alilohitaji la sh. milioni
26.
Aidha
imeelezwa kuwa dau hilo ni pesa aliyoihitaji Maximo kama mshahara kwa
mwezi, huku Maximo akiwa ni kati ya makocha 40 walioonyesha nia na
kuomba kukinoa kikosi hicho ambapo pia alikuwa ni miongoni mwa makocha
watatu waliobaki baada ya kuchujwa kutoka idadi hiyo kubwa.
Ikumbukwe
Kocha huyo Maximo alipokuwa akiinoa timu ya Taifa Stars, alikuwa
akilipwa kitita cha Sh. milioni 15 na Serikali, sasa kwa dau hilo
alilolihitaji kutoka Yanga, Yanga itaipiku serikali kwa kukubali kumlipa
dau hilo linalozidi dau alilokuwa akilipwa na Serikali au la. Tusubiri
tuone mwisho wa mchezo ni nani atakabidhiwa Kikosi hicho cha watoto wa
Jangwani.


Post a Comment