Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Makalla amshtaki Sumaye kwa JK

 
Naibu Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla (pichani), amemuomba Rais Jakaya Kikwete kutengua umiliki ardhi wa hekta 5000 wa Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye, wilayani Mvomero kutokana na kushindwa kuiendeleza.
 
Makalla alisema kuwa ameshaiandikia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imshauri Rais kutengua umiliki huo wa  Sumaye kupitia kikundi cha Katenda ili kurudishwa kwa wananchi.
 
Maeneo mengine aliyopendekeza yarudishwe kwa wananchi ni pamoja na ranchi ya Mkata  na Kipunguni katika kata ya Melela wilayani humo.
 
Makalla ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Mvomero, alisema hayo wakati akichangia hoja za migogoro ya ardhi iliyoibuliwa na wajumbe katika kikao cha kamati ya ushauri (RCC) ya mkoa wa Morogoro.
 
Alisema kuwa kuna mashamba mengi yanamilikiwa na vigogo akiwemo waziri mkuu huyo mstaafu kupitia kikundi hicho lakini yameshindwa kuendelezwa na kubaki mapori huku wananchi wakikosa maeneo ya kilimo.
 
“Sisi Mvomero tayari tumeshabaini hayo mashamba pori likiwemo la Sumaye na tumewandikia barua Wizara ya ardhi kumshauri Rais Kikwete kutengua umiliki wake ili wapewe wananchi wake,” alisema.
 
Awali Mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini, Innocent Kalogerezi, akielezea kwa kina suala la mashamba pori yanayomilikiwa na vigogo katika mkoa huo likiwemo la Mvomero alitaka kikao hicho kutoka na maazimio ya kuunda kamati itakayobaini mashamba pori ambayo hayaendelezwi.
 
Alisema kuwa kamati hiyo itakapobaini wamiliki wa mashamba pori bila kujali nyadhifa za viongozi mbalimbali wawasilishe kwa Rais Kikwete ili afute umiliki na kupewa wananchi.
 
Kalogerezi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Morogoro, alisema kupitia umoja wao wa wabunge wa mkoa huo watalizungumzia suala hilo katika bunge ili liweze kutoa maamuzi.
 
Alisema kuwa mkoa wa Morogoro umekuwa ukikabiliwa na migogoro ya wakulima na wafugaji kutokana na maeneo mengi kuhodhiwa bila kuendelezwa na vigogo.
 
“Lazima ifike mwisho kwa migogoro hii ya wakulima na wafugaji, tuunganishe nguvu ya pamoja bila kujali itikadi ya siasa kutetea mkoa wa Morogoro ambao kiasili ni mkoa wa kilimo,” alisema.
 
Aliwataka wajumbe wa kamati hiyo ya ushauri ya mkoa wa Morogoro, kufanya maamuzi ya kuzuia uingizaji wa wafugaji wapya pamoja na kutambua wingi wa mifugo na hatua ya kuipunguza iweze kufanyika na kuepusha mkoa kugeuka kuwa jangwa.
 
Naye Kaimu katibu wa Chama cha Demokrasia ma Maendeleo (Chadema), mkoa wa Morogoro, Boniface Ngonyani, aliunga mkono hoja ya wabunge hao wa CCM kwa hatua ya kumwandikia Rais Kikwete kutengua umiliki wa mashamba pori yanayomilikiwa na vigogo katika wilaya mbalimbali za mkoa wa Morogoro.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top