Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS KIKWETE ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi kutokana na kifo cha Diwani wa Kata ya Mchafukoge, Jijini Dar es Salaam na mbunge wa zamani wa Dodoma Mjini, Hashim Sagaf. Katika salaamu hizo, Rais Kikwete alisema kuwa amesikitishwa na kuhuzunishwa na kifo cha Sagaf, kilitokea juzi katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam na kuzikwa jana mjini Dar es Salaam.
             
“Nimepokea kwa huzuni na masikitiko taarifa za kifo cha Sagaf. Nilimfahamu Sagaf kwa miaka mingi. Alikuwa ni kiongozi hodari wa umma. Alikuwa raia mwaminifu kwa nchi yake na mzalendo wa kweli.”

“Nakutumia wewe Mheshimiwa Masaburi, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, salamu za dhati ya moyo wangu za rambirambi kuomboleza kifo cha Sagaf. Aidha, kupitia kwako, naomba uniwasilishie salamu zangu za pole nyingi kwa ndugu, jamaa na wanafamilia za Mheshimiwa Sagaf,” alisema Rais Kikwete katika rambirambi zake.

Katika hatua nyingine, Tanzania imefanya vizuri na kuonyesha mafanikio kuliko nchi nyingine yoyote duniani kati ya nchi nane zilikuwa zinashiriki Mpango wa Majaribio wa Kuuwezesha Mfumo wa Umoja wa Mataifa Kufanya Kazi kwa Pamoja.

MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top