Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Zitto ruksa kukata rufaa Chadema

Uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) umempelekea Zitto Kabwe (pichani) taarifa ya kikao cha Kamati Kuu kilichomvua madaraka yake ndani ya chama hicho ili aweze kukata rufaa.

Habari za kutoka ndani ya Chadema zinaeleza kuwa Kamati Kuu ya chama hicho ilifikia uamuzi huo wakati wa vikao vyake vilivyofanyika kati ya Januari 3 na 4, mwaka huu.

Kutokana na uamuzi huo, Zitto sasa ataweza kukata rufaa ya kupinga kuvuliwa madaraka kwenye Baraza Kuu la chama hicho.

Taarifa zinaeleza kuwa kamati hiyo ilimwagiza Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kumpatia mwenendo wa kikao Zitto ili aweze kukata rufaa.

Dk Slaa alithibitisha jana kuwa chama hicho tayari kimetuma muhtasari wa kikao hicho kwa Zitto, ambaye alikuwa anauhitaji hadi kufikia hatua ya kufungua mashtaka mahakamani.

Mwanasheria wa Zitto, Albert Msando alisema wamepokea barua hiyo na walikuwa wanajiandaa kukata rufaa.


“Ni kweli tumepokea taarifa ile na tulikuwa tuna fursa ya kuchagua kukata rufaa au la, lakini tumeisoma na tumeona tukate rufaa,” aliongeza Msando.

Alisema hatua hiyo, bado haitasimamisha kesi inayoendelea mahakamani, bali walalamikiwa sasa wana fursa ya kuitisha kikao cha Baraza Kuu na kupima kama wana haja ya kuendelea na kesi.

Gazeti hili limeshuhudia barua hiyo iliyotumwa kwa Zitto, Januari 20, 2014 ikiwa na namba ya kumbukumbu namba C/HQ/ADM/KK/08/40.

Katika barua hiyo, Zitto aliarifiwa kuwa Kamati Kuu ya Chadema katika kikao chake cha Januari 3 na 4, 2014 kiliandaa taarifa kamili ya mwenendo wa shauri lake.

“Kwa kuwa Kamati Kuu ilikuwa ikitambua umuhimu wa yeye kupewa nakala za mwenendo huo wa uamuzi wa kikao hicho, ilimwagiza Katibu Mkuu wa Chadema kumpatia Zitto nakala za mwenendo wa kikao.

Barua hiyo inaeleza kuwa uamuzi huo ulifikiwa baada ya taarifa ya Zitto iliyoeleza nia yake ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Kamati Kuu, wa kumvua nyadhifa zake.
 
MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top