Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CCM YAPATA PIGO KUFUATIA KIFO CHA KADA WAKE MAARUFU MKOANI SHINYANGA


Chama Cha Mapinduzi  mkoani Shinyanga kimepata pigo Kufuatia kifo cha mmoja wa makada wake maarufu ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa CCM katika kata ya Iselamagazi wilayani Shinyanga, Paul Zephania (61) aliyefariki dunia juzi baada ya kuugua malaria tarehe 14 mwezi huu na kufariki tarehe 18 mwezi huu saa 12 jioni.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa CCM mkoani Shinyanga, Khamis Mgeja amesema CCM itamkumbuka Zephania kwa  juhudi zake za uimarishaji wa chama alizokuwa akizifanya wakati wa uhai wake na kwamba
 ameacha pengo kubwa mbalo litachukua muda kuzibika kutokana na shughuli alizokuwa akizifanya ndani ya chama.
Akiongoza mazishi ya kada huyo kijijini kwake Iselamagazi jana, Mgeja alisema  marehemu Zephania alijiunga na chama cha mapinduzi tangu mwaka 1978 na mwaka 2002 alikuwa katibu  wa tawi  CCM wilayani humo, na mnamo mwaka 2012 alikuwa mwenyekiti wa kata ya Iselamagazi hadi mauti kumfika.
 Alisema CCM imepata pigo kubwa kwa kuondokewa na kiongozi wetu shupavu ambaye amekitumikia Chama kwa mda mrefu sana (36),tangu ajiunge na CCM alikuwa mchapa kazi na haja wahi kulalamikiwa na mtu yeyote na ndio maana mnaona maelfu ya watu Mmekuja kumpumzisha kwenye makazi yake ya milele kwa sababu alikuwa mtu wa watu.


Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top