Mahakama
ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Chunya mwishoni mwa wiki iliwahukumu watu
tisa kwenda jela jumla kwa miaka 270 baada ya kupatikana na hatia ya
wizi wa kutumia silaha.
Washtakiwa
hao ni Samweli Sarehe (40), Bahati Kenson (29), Aulesi Andason (28) na
Ayubu Swila (24), wote wakazi wa Mbalizi Wilaya ya Mbeya Vijijini.
Wengine
ni Mathias Simfukwe (31), Pascal Simchimba (27) wote wakazi wa Kijiji
cha Kanga Wilaya ya Chunya, Tegemea Kenya (27) mkazi wa Kijiji cha
Mjele, Shukuru Mwakatumbula (27) wa Ifumbo na Maleba Kindagilo (46) wa
Lupa, Chunya.
Awali,
ilielezwa mahakamani hapo na mwendesha mashtaka wa polisi, Raymond
Lukomwa kuwa washtakiwa wote kwa pamoja walifikishwa mahakamani hapo
Desemba 27, 2013 kwa kosa moja la wizi wa kutumia silaha kinyume na
Kifungu cha 287A cha Sheria ya Adhabu, Sura ya 16 iliyofanyiwa
marekebisho 2012.
Alidai
kuwa washtakiwa walifanya kosa hilo Desemba 14, 2013 katika eneo la
Kasangakanyika ambako waliiba vipimo vitano vya dhahabu vyenye thamani
ya Sh58 milioni na fedha tasilimu Sh6milioni, mali ya Paul Sinjale (44)
na kwamba katika wizi huo walitumia bunduki aina ya shortgun.
Akisoma
hukumu hiyo, Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Chunya, Desdeli Magezi alisema
kwa mujibu wa Kifungu cha Tano (A) (ii) cha Sheria ya Adhabu, Sura ya
90 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 wote kwa pamoja wanahukumiwa
kifungo cha miaka 270 na kila mmoja atatumikia kifungo cha miaka 30
jela.



Post a Comment